-
Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye UpendoMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
13. Waangalizi na Wakristo wote watatoa hesabu kwa nani na kwa njia gani?
13 Sababu ya tatu inayotufanya tushirikiane kwa kupenda na waangalizi ni kwamba wanatulinda “kama wale watakaotoa hesabu.” Waangalizi wanakumbuka kwamba wao ni wachungaji wadogo, wanaotumika chini ya Wachungaji wa kimbingu, Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Ezekieli 34:22-24) Yehova ndiye Mmiliki wa kondoo, ambao ‘aliwanunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe,’ Naye atawatoza hesabu waangalizi waliowekwa rasmi kwa sababu ya jinsi wanavyolitendea kundi Lake, ambalo linapaswa kutendewa “kwa wororo.” (Matendo 20:28, 29) Kwa hiyo, sote tutatoa hesabu kwa Yehova kulingana na jinsi tunavyoitikia mwelekezo wake. (Waroma 14:10-12) Kuwatii wazee waliowekwa rasmi kunathibitisha pia kwamba tunamnyenyekea Kristo, Kichwa cha kutaniko.—Wakolosai 2:19.
-
-
Kujitiisha kwa Unyenyekevu Chini ya Wachungaji Wenye UpendoMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 1
-
-
16. Ikiwa mzee hafanyi mambo kupatana na mwelekezo, kwa nini hiyo si sababu ya kutufanya tuasi?
16 Nyakati nyingine, huenda mzee akafanya mambo kwa njia ambayo haipatani na mwelekezo wa jamii ya mtumwa mwaminifu na Baraza lake Linaloongoza. Akiendelea kufanya hivyo, atatozwa hesabu na Yehova, “mchungaji na mwangalizi wa nafsi [zetu].” (1 Petro 2:25) Lakini hatupaswi kutumia makosa au kasoro yoyote ya wazee fulani kuwa kisingizio cha kutojitiisha chini yao. Yehova habariki kutotii na uasi.—Hesabu 12:1, 2, 9-11.
-