Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nilivutiwa na Watu Wazee Wenye Hekima
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
    • NILIPOKABILI JARIBU LINGINE

      Mimi, Arne, na Gary tulikuwa na maisha ya familia yenye furaha. Baada ya muda Arne alipanua nyumba yetu ili tuishi pamoja na wazazi wangu waliozeeka. Hata hivyo, baada ya miaka sita ya ndoa, tulipata pigo lingine tofauti lenye kushtua. Arne aligunduliwa kuwa na kansa ya ubongo. Nilimtembelea hospitalini kila siku alipokuwa akipokea tiba ya miale kwa muda mrefu. Kwa muda fulani, ilionekana ni kwamba alikuwa anapata nafuu; kisha hali yake ikazorota na akapata ugonjwa wa kupooza. Niliambiwa kwamba angeishi kwa majuma machache tu. Hata hivyo, Arne hakufa. Mwishowe alirudi nyumbani, ambako niliendelea kumtunza hadi afya yake ilipoboreka. Baada ya muda, aliweza kutembea tena na kurudia utendaji wake akiwa mzee wa kutaniko. Mtazamo wake wa furaha na ucheshi wake ulimsaidia kupata nafuu na hivyo ikawa rahisi zaidi kwangu kuendelea kumtunza.

      Baada ya miaka mingi, mwaka wa 1986, afya ya Arne ilizorota tena. Tayari wazazi wangu walikuwa wamekufa, kwa hiyo tukahamia kwenye Milima ya Blue nje ya jiji la Sydney, karibu zaidi na marafiki wetu. Baadaye, Gary alimwoa Karin, dada mzuri sana wa kiroho, na wakapendekeza kwamba sote wanne tuishi katika nyumba moja. Baada ya miezi michache, sote tulihamia katika nyumba iliyokuwa karibu sana na mahali ambapo mimi na Arne tulikuwa tukiishi zamani.

      Kwa muda wa miezi 18 ya mwisho ya maisha yake, Arne hakutoka kitandani na alihitaji kutunzwa daima. Kwa kuwa nilikaa nyumbani kwa muda mrefu wakati huo, nilitumia saa mbili kila siku kujifunza Biblia na machapisho ya Biblia. Katika vipindi hivyo vya kujifunza, nilipata mashauri mengi ya hekima kuhusu jinsi ya kukabiliana na hali yangu. Pia, nilionyeshwa upendo kwa kutembelewa na waliozeeka katika kutaniko letu, baadhi yao walikuwa wamevumilia majaribu kama yangu. Ziara zao zilinitia moyo kwelikweli! Arne alikufa mnamo Aprili 2003 akiwa na tumaini hakika la ufufuo.

  • Nilivutiwa na Watu Wazee Wenye Hekima
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
    • [Picha katika ukurasa wa 16]

      Nikimtunza Arne alipokuwa mgonjwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki