-
Kuwatembelea Ndege Waliokuwa HatariniAmkeni!—2004 | Aprili 8
-
-
Makao ya Viumbe
Hifadhi ya Viumbe ya Bandari ya Castle iko karibu na visiwa vikuu vya Bermuda, vilivyo katika Bahari ya Atlantiki, kilometa 900 hivi mashariki mwa North Carolina, Marekani. Kisiwa cha Nonsuch ndicho kikubwa zaidi kati ya visiwa tisa vidogo ambavyo ni sehemu ya hifadhi hiyo. Kisiwa cha Nonsuch kina ukubwa wa ekari 15 na kiko mashariki kabisa mwa Bermuda. Chini ya usimamizi wa Dakt. Wingate, kisiwa hicho kilifanywa kuwa makao ya viumbe ili hatimaye mimea na wanyama wa asili waliosalia wa Bermuda wahifadhiwe.
-
-
Kuwatembelea Ndege Waliokuwa HatariniAmkeni!—2004 | Aprili 8
-
-
Dakt. Wingate anajibu: “Mwaka wa 1906, Louis Mowbray, mtaalamu wa vitu vya asili, alimpata ndege wa ajabu akiwa hai kwenye kisiwa kimoja kwenye Bandari ya Castle. Hatimaye alitambuliwa kuwa ndege wa cahow. Baadaye, mwaka wa 1935, kifaranga wa cahow alipatikana akiwa amekufa baada ya kugonga mnara wa taa. Na mwaka wa 1945, cahow mkubwa alipatikana akiwa amekufa kwenye ufuo wa Kisiwa cha Cooper, Bermuda. Huo ulikuwa uthibitisho uliotosha kuwafanya watafiti kutafuta ndege wengine. Kikundi cha watafiti kiliongozwa na Dakt. Robert Cushman Murphy wa Hifadhi ya Marekani ya Vitu vya Asili, na Louis S. Mowbray, msimamizi wa Hifadhi ya Serikali ya Viumbe wa Baharini ya Bermuda, ambaye ni mwana wa Louis Mowbray aliyempata yule cahow mwaka wa 1906.”
Dakt. Wingate anatabasamu anapoeleza: “Lilikuwa pendeleo kubwa kuombwa nijiunge na kikundi hicho, hasa kwa sababu nilikuwa mwanafunzi tu mwenye umri wa miaka 15 na nilipendezwa sana na ndege! Jumapili hiyo ya Januari 28, 1951, ilikuwa siku ambayo ilibadili maisha yangu. Sitasahau kamwe furaha ya Dakt. Murphy wakati yeye na Mowbray walipofanikiwa kumshika cahow akiwa hai katika nyufa yenye kina kirefu! Punde baadaye, serikali ikafanya visiwa vidogo vya Bandari ya Castle kuwa hifadhi ya cahow. Kisiwa cha Nonsuch kikawa sehemu ya hifadhi hiyo mwaka wa 1961, na mwaka uliofuata, mimi na mke wangu tulihamia huko ili niwe mtunzaji wa hifadhi hiyo.”
-