Mjadala Kuhusu Mashahidi wa Yehova Waonyeshwa Kwenye Televisheni
Mnamo mwaka wa 2000 na 2001, Mashahidi wa Yehova walishambuliwa katika nchi ya Georgia. Nchi hiyo ilikuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti hapo awali. Kituo kimoja maarufu cha televisheni nchini Georgia kilionyesha mjadala kati ya mwanasiasa na profesa mmoja. Mwanasiasa huyo alitaka Mashahidi wapigwe marufuku, na profesa huyo alikuwa ameteuliwa na mahakama kufanya utafiti kuhusu vichapo vya Mashahidi.
Akijibu mashtaka mengi kuhusu imani ya Mashahidi, profesa huyo alisema kwamba madai ya mwanasiasa huyo hayakuwa na uthibitisho wowote. Kisha akainua kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, ili watazamaji wakione, na kusema hivi: ‘Kitabu hiki kinaonyesha yale ambayo Mashahidi wa Yehova wanaamini.’
Halafu profesa huyo akasoma fungu la kwanza katika kitabu hicho, ambalo linamalizia kwa kusema hivi: “Hata hivyo, kwa wengi, maisha huonekana yakitokeza tatizo moja zito baada ya jingine. Ikiwa imekuwa hivyo kwako, jipe moyo.”
Kitabu hicho kinaonyesha majibu ya Biblia kwa maswali ambayo watu wengi huuliza. Kwa mfano, baadhi ya vichwa vilivyomo ni: “Mungu wa Kweli Ni Nani?,” “Sababu Gani Tunazeeka na Kufa?,” na “Sababu Gani Mungu Huruhusu Kuteseka?”
Je, ungependa kupokea nakala ya kitabu hicho chenye kurasa 192 ili wewe mwenyewe ukichunguze? Unaweza kuomba nakala ya kichapo hicho kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nitumieni kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.