Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2000—Je, Ni Mwaka wa Pekee?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Mwaka wa 2000 ni wa maana hata zaidi kwa wafuasi wa dini fulani-fulani. Wanasadiki kwamba katika mwaka ujao au baadaye kidogo, Yesu atarudi kwenye Mlima wa Mzeituni nayo vita ya Har–Magedoni, ambayo imetajwa katika kitabu cha Ufunuo, itapiganwa katika bonde la Megido. (Ufunuo 16:14-16) Kwa kutarajia matukio hayo, mamia ya wakazi wa Marekani wanauza makao yao na karibu mali zao zote na kuhamia Israeli. Kwa manufaa ya wowote wale wasioweza kuacha makao yao, inasemekana kwamba Mweneza-evanjeli mmoja mashuhuri wa Marekani ameahidi kutangaza kurudi kwa Yesu kupitia televisheni ya rangi!

  • Milenia ya Tatu Inaanza Lini?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Je, jambo hilo ni la maana? Kwa mfano, je, kuanza kwa milenia ya tatu kungekuwa mwanzo wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo, unaotajwa katika kitabu cha Ufunuo? La. Biblia haionyeshi popote uhusiano wowote kati ya milenia ya tatu na Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo.

      Yesu aliwaonya wafuasi wake dhidi ya kukisia tarehe. Aliwaambia wanafunzi wake: “Si juu yenu kupata ujuzi wa nyakati au majira ambayo Baba ameweka katika mamlaka yake mwenyewe.” (Matendo 1:7) Mapema kidogo, Yesu alifunua kwamba wakati huo hata yeye hakujua wakati ambapo Mungu angetekeleza hukumu juu ya mfumo huu mwovu, akiuandalia nafasi Utawala wa Milenia wa Kristo. Yeye alisema: “Kuhusu siku hiyo na saa hiyo hakuna mtu ajuaye, wala hao malaika wa mbingu wala Mwana, ila Baba tu.”—Mathayo 24:36.

      Je, ni jambo linalopatana na akili kutarajia kwamba Kristo atarudi miaka 2,000 kamili tangu azaliwe akiwa mwanadamu? La, sivyo. Ni lazima Yesu awe alijua tarehe yake ya kuzaliwa. Naye bila shaka alijua jinsi ya kuhesabu miaka 2,000 tangu tarehe hiyo. Hata hivyo, hakujua siku wala saa ya kuja kwake. Ni wazi kwamba haingekuwa rahisi hivyo kubainisha tarehe ya kurudi kwake! Baba ndiye aliyekuwa na mamlaka juu ya ‘nyakati na majira’—yeye pekee ndiye ajuaye ratiba.

      Isitoshe, Yesu hakuwaamuru wafuasi wake wamngojee mahali fulani hususa. Hakuwaambia wakusanyike na kungoja, bali watawanyike hadi “sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” na kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote. Hajawahi kubatilisha amri hiyo.—Matendo 1:8; Mathayo 28:19, 20.

      Je, Matumaini Yao ya Milenia Yataambulia Patupu?

      Hata hivyo, baadhi ya watu wenye itikadi kali za kidini wana matumaini makubwa kuhusu mwaka wa 2000. Wanaamini kwamba katika miezi kadhaa ijayo, sehemu fulani za kitabu cha Ufunuo zitatimizwa kihalisi. Kwa kweli, wanaona kuwa wao binafsi watahusika katika utimizo huo. Kwa mfano, wao hutaja unabii uliorekodiwa kwenye Ufunuo 11:3, 7, 8, unaosimulia juu ya mashahidi wawili ambao wanatoa unabii katika “jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho laitwa Sodoma na Misri, ambako pia Bwana wao alitundikwa mtini.” Wanapomaliza kutoa ushahidi, mashahidi hao wawili wanauawa na hayawani-mwitu mkali atokaye katika abiso.

      Kwa mujibu wa ripoti moja katika gazeti la The New York Times Magazine la Desemba 27, 1998, kiongozi wa dini moja “amewaambia wafuasi wake kwamba yeye ni mmojawapo wa hao mashahidi wawili ambao wamejaliwa kutangaza kuharibiwa kwa dunia na kuja kwa Bwana—kisha Shetani awaue katika barabara za Yerusalemu.” Wenye mamlaka katika Israeli wana sababu ya kuwa na wasiwasi. Wanahofu kwamba watu fulani wenye itikadi kali za kidini wanaweza kujaribu “kutimiza” unabii huo kwa njia yao wenyewe—hata ikiwa hiyo yamaanisha kuchochea mapambano ya kutumia silaha! Hata hivyo, Mungu hahitaji “msaada” wa mwanadamu ili kutimiza kusudi lake. Unabii wote wa Biblia utatimizwa katika wakati wa Mungu na katika njia yake mwenyewe.

      Kitabu cha Ufunuo kiliandikwa “kwa njia ya ishara.” Kwa mujibu wa Ufunuo 1:1, Yesu alitaka kuwafunulia “watumwa wake” (wala si ulimwengu kwa ujumla) mambo ambayo lazima yatukie upesi. Ili kukielewa kitabu cha Ufunuo, watumwa, au wafuasi wa Yesu wangehitaji roho takatifu ya Mungu, ambayo Yehova huwapa wale wampendezao. Kama kitabu cha Ufunuo chapaswa kueleweka kihalisi, hata watu wasio na imani wangeweza kukisoma na kukielewa. Nao Wakristo hawangehitaji kusali kupata roho takatifu ili kukielewa.—Mathayo 13:10-15.

      Tumeona kwamba kulingana na uthibitisho wa Biblia, milenia ya tatu tangu Yesu azaliwe inaanza katika vuli ya 1999 na kwamba tarehe hiyo wala Januari 1, 2000, wala Januari 1, 2001, haina maana yoyote ya pekee.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki