-
Kwa Nini Yamerudi?Amkeni!—2003 | Mei 22
-
-
Mfano mmoja ni ugonjwa wa Lyme, ambao uligunduliwa mwaka wa 1975. Ugonjwa huo ulionekana kwanza huko Lyme, Connecticut, Marekani, na ndiyo sababu ulipewa jina hilo. Huenda bakteria inayosababisha ugonjwa huo iliingia Amerika Kaskazini miaka mia moja iliyopita kupitia kwa panya au mifugo waliokuwa ndani ya meli zilizotoka Ulaya. Kupe mdogo anayeitwa Ixodes anaponyonya damu ya mnyama mwenye ugonjwa huo, bakteria hudumu katika utumbo wa kupe huyo hadi anapokufa. Kupe huyo anaweza kueneza bakteria hizo anapomuuma mnyama mwingine au mwanadamu.
Kwa muda mrefu, ugonjwa wa Lyme umekuwa ukiwakumba hasa watu wanaoishi katika eneo lililo kaskazini-mashariki mwa Marekani. Katika eneo hilo, panya wenye miguu myeupe ndio huwa hasa na bakteria za ugonjwa wa Lyme. Panya hao pia hubeba kupe, hasa wale kupe wanaoendelea kukomaa. Kupe hao wakiisha kukomaa, wao huhamia kwenye miili ya mbawala. Kisha wao hujamiiana na kuwanyonya mbawala. Kupe wa kike akiisha kushiba damu, yeye huanguka chini ili kutaga mayai, kisha kupe wanaongezeka.
Hali Zinapobadilika
Wanyama na wadudu wamebeba viini kwa miaka mingi bila kuwaathiri wanadamu. Lakini hali zinapobadilika, ugonjwa ambao haukuwa ukienea unaweza kuenea kwa watu wengi wanaoishi katika eneo moja. Ni hali zipi zilizosababisha ugonjwa wa Lyme uenee?
Hapo zamani, mbawala hawakuwa wengi kwani wanyama fulani waliwawinda. Hivyo, wanadamu hawakuwa wakivamiwa sana na wale kupe wanaoishi kwenye miili ya mbawala. Wakati walowezi Wazungu walipokata misitu ili walime, mbawala na wanyama waliowawinda walihamia katika maeneo mengine. Lakini katikati ya miaka ya 1800, wakulima walihamia katika maeneo ya magharibi mwa Marekani. Basi, mashamba yakaachwa ukiwa, na msitu ukatokea tena. Mbawala wakarudi, lakini wale wanyama waliokuwa wanawawinda hawakurudi. Kwa hiyo, mbawala wakaongezeka sana, na kupe pia.
Muda fulani baadaye, bakteria ya ugonjwa wa Lyme ikaibuka, na ikadumu mwilini mwa wanyama kwa makumi ya miaka kabla ya wanadamu kuambukizwa. Hata hivyo, watu walianza kujenga nyumba karibu na msitu huo, na watoto na watu wazima wengi wakahamia katika eneo hilo lenye kupe. Kupe wakaanza kuwanyonya wanadamu, na wanadamu wakapata ugonjwa wa Lyme.
-
-
Kwa Nini Yamerudi?Amkeni!—2003 | Mei 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 7]
Kupe wanaoishi kwenye miili ya mbawala (picha kubwa kulia) wanawaambukiza wanadamu ugonjwa wa Lyme
Kushoto hadi kulia: kupe wa kike aliyekomaa, wa kiume aliyekomaa, na mtoto wa kupe, wote wana ukubwa wa kawaida
[Hisani]
All ticks: CDC
-