-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kuandaa Msaada wa Kimwili, Kiroho, na Kihisia. Mara moja, ofisi ya tawi ya Japani ilipanga Halmashauri tatu za Kutoa Misaada na wawakilishi wa ofisi ya tawi walitumwa tena na tena katika maeneo yaliyoathiriwa. Waangalizi wa eneo Geoffrey Jackson na Izak Marais kutoka makao makuu walipoitembelea nchi hiyo mwezi wa Mei, vilevile walikutana na ndugu na dada kutoka maeneo yaliyoathiriwa zaidi. Mkutano wa pekee kwa ajili ya makutaniko yaliyoathiriwa ulipangwa, Majumba ya Ufalme 21 yaliunganishwa kwa simu na hivyo ndugu wapatao 2,800 wakahakikishiwa kwamba ndugu zao ulimwenguni pote wanawapenda na wanawahangaikia.
Ndugu wa Halmashauri za Kutoa Misaada na wajitoleaji wengine wamefanya kazi kwa bidii. Vitu vilivyohitajiwa mara moja ni chakula, maji, na fueli. Halmashauri za misaada zilifanya pia mipango ya kutuma nguo za vipimo mbalimbali kwa makutaniko yaliyoathiriwa. Maeneo ya mikutano yalikuwa kama “maduka ya kuuzia nguo” ambapo ndugu wangepata mavazi waliyohitaji.
Ndugu na dada walioathiriwa walifurahi kama nini kuona jinsi Yehova alivyotosheleza mahitaji yao ya kimwili na kihisia! Walitiwa nguvu hasa walipohudhuria mikutano ya Kikristo. Dada mmoja kutoka eneo la msiba aliandika hivi, “Ninapata amani ya akili ninapohudhuria mikutano. Mikutano ndiyo uti wa mgongo wa maisha yangu ya Kikristo.”
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 22]
Juu: Wajitoleaji wakibeba vifusi kutoka nyumba ya ndugu fulani huko Shibata, Miyagi
[Picha katika ukurasa wa 22]
Kushoto: Mshiriki wa Halmashauri ya Tawi akitoa hotuba katika nyumba ya ndugu huko Rikuzentakata
[Picha katika ukurasa wa 22]
Chini: Wajitoleaji wakiwatayarishia wahudhuriaji chakula cha mchana wakati wa kusanyiko la pekee katika eneo lililoathiriwa
-