-
“Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii” Wakusanyika kwa ShangweMnara wa Mlinzi—2003 | Januari 15
-
-
Hotuba yenye kichwa “Vijana—Pangeni Maisha Yenu ya Wakati Ujao Katika Tengenezo la Yehova” ilijibu swali hili: Kijana anawezaje kufaidika kabisa maishani? Hiyo haiwezekani kwa kutafuta fedha, mali, na umaarufu. Muumba wetu huwasihi vijana kwa upendo wamkumbuke wakiwa wangali vijana. Msemaji alihoji baadhi ya vijana ambao wamejitahidi katika utumishi wa Kikristo, na tuliweza kuona shangwe yao. Na ilinufaisha kama nini kupokea trakti mpya, Vijana—Mtatumiaje Maisha Yenu?, iliyokusudiwa kusaidia vijana Mashahidi waweke msingi wa wakati ujao wa milele katika tengenezo la Yehova!
-
-
“Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii” Wakusanyika kwa ShangweMnara wa Mlinzi—2003 | Januari 15
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26]
Mwongozo wa Kiroho kwa Vijana
Katika siku ya tatu ya kusanyiko, trakti ya pekee yenye kichwa Vijana—Mtatumiaje Maisha Yenu? ilitolewa. Trakti hii mpya inayokusudiwa kusaidia vijana Mashahidi wafanye maamuzi yanayofaa kuhusu wakati wao ujao, inawapa mashauri ya Kimaandiko kuhusu jinsi ya kufanya utumishi wa Yehova uwe kazi yao ya maisha.
-