-
Baraka Kubwa Zaidi Kupitia Agano JipyaMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
Mataifa Yabarikiwa Kupitia Mbegu ya Abrahamu
5, 6. Katika utimizo wa msingi na wa kiroho wa agano la Kiabrahamu, ni nani aliye Mbegu ya Abrahamu, na ni taifa jipi lililokuwa la kwanza kupokea baraka kupitia yeye?
5 Yehova alimwahidi Abrahamu hivi: “Katika uzao wako [“mbegu yako,” NW] mataifa yote ya dunia watajibarikia.” (Mwanzo 22:18) Chini ya agano la zamani, wageni wengi wenye tabia-pole walibarikiwa kupitia ushirikiano wao na Israeli, mbegu ya kitaifa ya Abrahamu. Hata hivyo, katika utimizo wake wa kimsingi na wa kiroho, Mbegu ya Abrahamu ilikuwa mtu mmoja aliye mkamilifu. Paulo alieleza hilo aliposema hivi: “Ahadi zilisemwa kwa Abrahamu na kwa mbegu yake. Haisemi: ‘Na kwa hizo mbegu,’ kama katika kisa cha nyingi za namna hiyo, bali kama katika kisa cha moja: ‘Na kwa mbegu yako,’ ambaye ni Kristo.”—Wagalatia 3:16.
6 Ndiyo, Yesu ndiye Mbegu ya Abrahamu, na kupitia Yeye mataifa hupokea baraka iliyo bora zaidi kuliko yoyote ambayo iliwezekana kwa Israeli la kimwili. Kwa kweli, taifa la kwanza kupokea baraka hiyo lilikuwa Israeli lenyewe. Mara baada ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K., mtume Petro alikiambia kikundi cha Wayahudi hivi: “Nyinyi ndio wana wa manabii na wa agano ambalo Mungu aliagana pamoja na baba zenu wa zamani, akimwambia Abrahamu, ‘Na katika mbegu yako familia zote za dunia zitabarikiwa.’ Baada ya kumwinua Mtumishi wake, Mungu alimtuma kwenu kwanza ili kuwabariki nyinyi kwa kugeuzia mbali kila mmoja kutoka kwenye vitendo vyenu viovu.”—Matendo 3:25, 26.
7. Ni mataifa yapi yaliyobarikiwa kupitia Yesu, Mbegu ya Abrahamu?
7 Punde si punde hiyo baraka ilipanuliwa kuwafikia Wasamaria kisha kuwafikia Wasio-Wayahudi. (Matendo 8:14-17; 10:34-48) Wakati fulani kati ya mwaka wa 50 na wa 52 W.K., Paulo aliwaandikia Wakristo waliokuwa Galatia katika Asia Ndogo hivi: “Andiko, likitangulia kuona kwamba Mungu angetangaza watu wa mataifa kuwa waadilifu kwa sababu ya imani, lilitangaza habari njema kimbele kwa Abrahamu, yaani: ‘Kupitia wewe mataifa yote yatabarikiwa.’ Kwa sababu hiyo wale washikamanao sana na imani wanakuwa wenye kubarikiwa pamoja na Abrahamu mwaminifu.” (Wagalatia 3:8, 9; Mwanzo 12:3) Ijapokuwa Wakristo wengi katika Galatia walikuwa “watu wa mataifa,” walibarikiwa kupitia Yesu kwa sababu ya imani yao. Katika njia gani?
8. Kwa Wakristo wa siku ya Paulo, kubarikiwa kupitia Mbegu ya Abrahamu kulitia ndani nini, na mwishowe, ni wangapi waliopokea baraka hiyo?
8 Paulo aliwaambia hivi Wakristo Wagalatia, hata wawe wa malezi gani: “Ikiwa nyinyi ni wa Kristo, kwa kweli nyinyi ni mbegu ya Abrahamu, warithi kuhusiana na ahadi.” (Wagalatia 3:29) Kwa Wagalatia hao, baraka kupitia Mbegu ya Abrahamu ilitia ndani kuwa kwao washiriki katika agano jipya na pia kuwa warithi-wenzi wa Yesu, washiriki pamoja na Yesu katika mbegu ya Abrahamu. Hatujui idadi ya watu wa Israeli la kale. Twajua tu kwamba lilikuja kuwa “kama mchanga wa pwani kwa wingi.” (1 Wafalme 4:20) Hata hivyo, twajua idadi ya mwisho ya washiriki wa Yesu katika hiyo mbegu ya kiroho—144,000. (Ufunuo 7:4; 14:1) Washiriki hao 144,000 hutoka katika “kila kabila na ulimi na watu na taifa” la wanadamu na hushiriki katika kuwatolea wengine zaidi baraka za hilo agano la Kiabrahamu.—Ufunuo 5:9.
Unabii Uliotimizwa
9. Wale walio katika agano jipya huwaje na sheria ya Yehova ndani yao?
9 Alipotabiri juu ya agano jipya, Yeremia aliandika hivi: “Agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema BWANA; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika.” (Yeremia 31:33) Wale walio katika agano jipya wana sifa ya kumtumikia Yehova kwa sababu ya upendo. (Yohana 13:35; Waebrania 1:9) Sheria ya Yehova imeandikwa katika moyo wao, nao hutamani kwa bidii kufanya mapenzi yake. Ni kweli, katika Israeli la kale watu fulani waaminifu walipenda sana sheria ya Yehova. (Zaburi 119:97) Lakini wengi hawakuipenda. Lakini waliendelea kuwa sehemu ya hilo taifa. Hakuna yeyote awezaye kuendelea kuwa katika agano jipya ikiwa sheria ya Mungu haijaandikwa katika moyo wake.
10, 11. Kwa wale walio katika agano jipya, Yehova ‘hupataje kuwa Mungu wao,’ na wote watamjuaje?
10 Yehova aliongezea kusema hivi kuhusu wale walio katika agano jipya: “Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.” (Yeremia 31:33) Katika Israeli la kale wengi waliabudu miungu ya mataifa, lakini waliendelea kuwa Waisraeli. Kwa msingi wa agano jipya, Yehova alitokeza taifa la kiroho, “Israeli wa Mungu,” ili kuchukua mahali pa Israeli la kimwili. (Wagalatia 6:16; Mathayo 21:43; Waroma 9:6-8) Hata hivyo, hakuna mtu ambaye huendelea kuwa sehemu ya taifa jipya la kiroho akiacha kumwabudu Yehova na kumwabudu yeye peke yake.
11 Yehova alisema hivi pia: “Watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao.” (Yeremia 31:34) Katika Israeli, wengi walimpuuza Yehova tu, wakisema hivi kumhusu: “BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.” (Sefania 1:12) Hakuna yeyote aendeleaye kuwa sehemu ya Israeli wa Mungu akimpuuza Yehova au kuchafua ibada safi. (Mathayo 6:24; Wakolosai 3:5) Waisraeli wa kiroho ni “watu wamjuao Mungu wao.” (Danieli 11:32) Wao hupendezwa na ‘kuendelea kutwaa ujuzi juu ya Mungu pekee wa kweli, na juu ya Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Kumjua Yesu huongezea kina ujuzi wao juu ya Mungu kwa kuwa, katika njia ya pekee, Yesu “ndiye ambaye amemweleza [Mungu].”—Yohana 1:18; 14:9-11.
12, 13. (a) Ni juu ya msingi gani Yehova husamehe dhambi za wale walio katika agano jipya? (b) Kwa habari ya msamaha wa dhambi, ni jinsi gani agano jipya ni lenye ubora kuliko agano la zamani?
12 Mwishowe, Yehova aliahidi hivi: “Nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yeremia 31:34b) Sheria ya Musa ilitia ndani mamia ya kanuni zilizoandikwa ambazo Waisraeli walitakiwa kuzitii. (Kumbukumbu la Torati 28:1, 2, 15) Wote waliovunja Sheria walitoa dhabihu ili kufunika dhambi zao. (Mambo ya Walawi 4:1-7; 16:1-31) Wayahudi wengi walikuja kuamini kwamba wangeweza kuwa waadilifu kupitia kazi zao wenyewe kulingana na Sheria. Ingawa hivyo, Wakristo hung’amua kwamba hawawezi kamwe kuchuma uadilifu kwa kazi zao wenyewe. Hawawezi kuepuka kufanya dhambi. (Waroma 5:12) Chini ya agano jipya, msimamo mwadilifu mbele ya Mungu wawezekana tu kwa msingi wa dhabihu ya Yesu. Hata hivyo, msimamo huo ni zawadi, fadhili isiyostahiliwa kutoka kwa Mungu. (Waroma 3:20, 23, 24) Yehova bado hudai utii kutoka kwa watumishi wake. Paulo asema kwamba walio katika agano jipya wako “chini ya sheria kuelekea Kristo.”—1 Wakorintho 9:21.
13 Kwa sababu hiyo, kwa Wakristo pia kuna dhabihu kwa ajili ya dhambi, lakini ambayo ni yenye thamani zaidi sana kuliko dhabihu mbalimbali chini ya agano la Sheria. Paulo aliandika hivi: “Kila kuhani [chini ya agano la Sheria] huenda mahali pa kazi kutoka siku hadi siku kutoa utumishi wa watu wote na kutoa dhabihu zilezile mara nyingi, kwa kuwa hizi haziwezi wakati wowote kamwe kuziondolea mbali dhambi kabisa. Lakini [Yesu] alitoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi daima dawamu na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu.” (Waebrania 10:11, 12) Kwa kuwa Wakristo katika agano jipya hudhihirisha imani katika dhabihu ya Yesu, Yehova huwatangaza kuwa waadilifu, bila dhambi, na hivyo kuwa katika hali ya kutiwa mafuta kuwa wana wake wa kiroho. (Waroma 5:1; 8:33, 34; Waebrania 10:14-18) Wafanyapo dhambi kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu, wao waweza kuomba msamaha wa Yehova, na kwa msingi wa dhabihu ya Yesu, Yehova huwasamehe. (1 Yohana 2:1, 2) Hata hivyo, wakichagua mwendo wa kufanya dhambi kimakusudi, wao hupoteza msimamo wao mwadilifu na lile pendeleo la kuwa washiriki katika agano jipya.—Waebrania 2:2, 3; 6:4-8; 10:26-31.
Agano la Zamani na Jipya
14. Ni tohara gani iliyotakwa chini ya agano la Sheria? chini ya agano jipya?
14 Watu wa kiume katika agano la zamani walitahiriwa ikiwa ishara kwamba walikuwa chini ya Sheria. (Mambo ya Walawi 12:2, 3; Wagalatia 5:3) Baada ya kutaniko la Kikristo kuanza, watu fulani walihisi kwamba Wakristo wasio Wayahudi walipaswa pia kutahiriwa. Lakini mitume na wazee katika Yerusalemu, wakiongozwa na Neno la Mungu na roho takatifu, walifahamu kwamba jambo hilo halikuwa lazima. (Matendo 15:1, 5, 28, 29) Miaka michache baadaye, Paulo alisema hivi: “Yeye si Myahudi aliye hivyo kwa nje, wala tohara si ile ambayo ni ya nje juu ya mwili. Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani, na tohara yake ni ile ya moyo kwa roho, wala si kwa mfumo fulani wa sheria iliyoandikwa.” (Waroma 2:28, 29) Hata kwa Wayahudi wa kimwili, tohara halisi haikuwa na thamani zaidi kiroho machoni pa Yehova. Kwa wale walio katika agano jipya, moyo, wala si mwili, lazima utahiriwe. Kila kitu wakifikiriacho, tamaa, na kichocheo kisichopendeza au kisicho safi machoni pa Yehova lazima kikataliwe mbali.a Wengi leo ni ushuhuda ulio hai kwamba roho takatifu ina nguvu ya kugeuza namna za kufikiri katika njia hiyo.—1 Wakorintho 6:9-11; Wagalatia 5:22-24; Waefeso 4:22-24.
15. Israeli la kimwili na Israeli wa Mungu hulinganaje kwa habari ya utawala wa kifalme?
15 Katika mpango wa agano la Sheria, Yehova alikuwa ndiye Mfalme wa Israeli, na baada ya muda alidhihirisha enzi kuu yake kupitia wafalme wa kibinadamu katika Yerusalemu. (Isaya 33:22) Yehova pia ndiye Mfalme wa Israeli wa Mungu, Israeli wa kiroho, na tangu 33 W.K., amewatawala kupitia Yesu Kristo, aliyepokea “mamlaka yote mbinguni na juu ya dunia.” (Mathayo 28:18; Waefeso 1:19-23; Wakolosai 1:13, 14) Leo, Israeli wa Mungu humtambua Yesu kuwa Mfalme wa Ufalme wa kimbingu wa Mungu, uliosimamishwa mwaka wa 1914. Yesu ni Mfalme bora zaidi kuliko hata walivyokuwa Hezekia, Yosia, na wafalme wengine waaminifu wa Israeli la kale.—Waebrania 1:8, 9; Ufunuo 11:15.
16. Israeli wa Mungu ni ukuhani wa aina gani?
16 Israeli halikuwa ufalme tu bali pia lilikuwa na ukuhani uliotiwa mafuta. Katika 33 W.K., Israeli wa kiroho wa Mungu walichukua mahali pa Israeli la kimwili na kuwa “mtumishi” wa Yehova, “mashahidi” wake. (Isaya 43:10) Tangu wakati huo maneno ya Yehova kwa Israeli yaliyorekodiwa kwenye Isaya 43:21 na Kutoka 19:5, 6 yalitumika kuhusu Israeli wa Mungu. Taifa jipya la kiroho la Mungu lilikuwa sasa “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya miliki ya pekee,” lenye daraka la ‘kutangaza kotekote sifa bora kabisa za Yehova.’ (1 Petro 2:9) Wote katika Israeli wa Mungu, wanaume kwa wanawake, hufanyiza jamii ya ukuhani. (Wagalatia 3:28, 29) Wakiwa sehemu ya pili ya mbegu ya Abrahamu, sasa wao husema hivi: “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake.” (Kumbukumbu la Torati 32:43) Wale wa Israeli wa kiroho walio duniani bado hufanyiza “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mathayo 24:45-47) Ni katika ushirikiano pamoja nao tu ndipo utumishi mtakatifu wenye kukubalika uwezapo kutolewa kwa Mungu.
Ufalme wa Mungu —Utimizo wa Mwisho
17. Wale walio katika agano jipya hupata kuzaliwa kwa namna gani?
17 Waisraeli waliozaliwa baada ya mwaka wa 1513 K.W.K. waliingia katika agano la Sheria wakati wa kuzaliwa. Wale ambao Yehova huingiza katika agano jipya pia hupata kuzaliwa—kwa habari yao, huko ni kuzaliwa kwa kiroho. Yesu alimtajia Farisayo Nikodemo jambo hilo aliposema hivi: “Kwa kweli kabisa mimi nakuambia, Isipokuwa yeyote azaliwe tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Wale wanafunzi 120 kwenye Pentekoste mwaka wa 33 W.K. ndio waliokuwa wanadamu wa kwanza wasio wakamilifu kupata kuzaliwa huko kupya. Wakiwa wametangazwa kuwa waadilifu chini ya agano jipya, walipokea roho takatifu ikiwa “arbuni ya kimbele” ya urithi wao wa kifalme. (Waefeso 1:14) ‘Walizaliwa kutokana na roho’ ili wapate kufanywa wana wa Mungu, kuzaliwa ambako kuliwafanya ndugu za Yesu na hivyo “warithi-washirika pamoja na Kristo.” (Yohana 3:6; Waroma 8:16, 17) ‘Kuzaliwa kwao tena’ kulifungulia njia matazamio ya ajabu.
18. Kuzaliwa tena hutayarishia njia matazamio gani ya ajabu kwa wale walio katika agano jipya?
18 Alipokuwa akipatanisha agano jipya, Yesu alifanya agano la ziada pamoja na wafuasi wake, akisema hivi: “Nafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu amefanya agano pamoja nami, kwa ajili ya ufalme.” (Luka 22:29) Agano hilo la Ufalme lilitayarishia njia utimizo wa ono lenye kutokeza, lililorekodiwa kwenye Danieli 7:13, 14, 22, 27. Danieli aliona “mmoja aliye mfano wa mwanadamu” akipewa mamlaka ya kifalme na “mzee wa siku,” Yehova Mungu. Kisha Danieli akaona kwamba “watakatifu wa[li]umiliki ufalme.” Yesu ndiye yule “aliye mfano wa mwanadamu” ambaye, mwaka wa 1914, alipokea Ufalme wa kimbingu kutoka kwa Yehova Mungu. Wanafunzi wake waliotiwa mafuta kwa roho ndio “watakatifu,” ambao hushiriki pamoja naye katika Ufalme huo. (1 Wathesalonike 2:12) Jinsi gani?
19, 20. (a) Kwa wale walio katika agano jipya, ahadi ya Yehova kwa Abrahamu itakuwa na utimizo gani wa mwisho, wenye utukufu? (b) Ni swali jipi la ziada lihitajilo kufikiriwa?
19 Kama Yesu, baada ya kifo chao, watiwa-mafuta hao hufufuliwa kutoka kwa wafu wakiwa viumbe wa roho wasioweza kufa ili kutumikia pamoja naye wakiwa wafalme na makuhani mbinguni. (1 Wakorintho 15:50-53; Ufunuo 20:4, 6) Ni tumaini lenye utukufu kama nini! “Nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia,” sio nchi ya Kanaani tu. (Ufunuo 5:10) Je, ‘watamiliki milango ya adui zao’? (Mwanzo 22:17) Ndiyo, na katika njia yenye kukata maneno, washuhudiapo kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa, kahaba wa kidini mwenye uhasama, na watiwa-mafuta hao waliofufuliwa washirikianapo na Yesu katika kuchunga mataifa “kwa fimbo ya chuma” na katika kuponda kichwa cha Shetani. Hivyo watakuwa na sehemu katika kutimiza sehemu ya mwisho kabisa ya ule unabii kwenye Mwanzo 3:15.—Ufunuo 2:26, 27; 17:14; 18:20, 21; Waroma 16:20.
-
-
Kondoo Wengine na Agano JipyaMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
1. (a) Kulingana na ono la Yohana, nini hutimizwa huku pepo za hukumu ya Yehova zikizuiwa? (b) Yohana aliona umati upi wenye kutokeza?
KATIKA ono la nne kwenye kitabu cha Ufunuo, mtume Yohana aliona pepo zenye kuharibu za hukumu ya Yehova zimezuiwa huku kutiwa muhuri kwa washiriki wote wa “Israeli wa Mungu” kukikamilishwa. Hao ndio wa kwanza kubarikiwa kupitia Yesu, sehemu iliyo kuu ya mbegu ya Abrahamu. (Wagalatia 6:16; Mwanzo 22:18; Ufunuo 7:1-4)
-
-
Kondoo Wengine na Agano JipyaMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
3. Wakristo watiwa-mafuta na kondoo wengine hutofautianaje kuhusiana na agano jipya?
3 Kwa wale 144,000, baraka ya agano la Kiabrahamu hutekelezwa kupitia agano jipya. Wakiwa washiriki katika agano hilo, wao huja “chini ya fadhili isiyostahiliwa” na “chini ya sheria kuelekea Kristo.” (Waroma 6:15; 1 Wakorintho 9:21) Kwa sababu hiyo, wale washiriki 144,000 wa Israeli wa Mungu ndio pekee ambao wameshiriki mifano ifaavyo wakati wa Ukumbusho wa kifo cha Yesu, na Yesu alifanya agano lake kwa ajili ya Ufalme pamoja nao pekee. (Luka 22:19, 20, 29)
-
-
Kondoo Wengine na Agano JipyaMnara wa Mlinzi—1998 | Februari 1
-
-
5 Katika siku yetu, ‘wageni ambao wameandamana na BWANA’ ni ule umati mkubwa. Hao humhudumu Yehova kwa ushirikiano na Israeli wa Mungu. (Zekaria 8:23) Wao hutoa dhabihu zilezile zenye kukubalika watoazo Israeli wa Mungu. (Waebrania 13:15, 16) Wao huabudu katika hekalu la Mungu la kiroho, “nyumba [yake] ya sala.” (Linganisha Ufunuo 7:15.) Je, wao hushika Sabato ya kila juma? Wala watiwa-mafuta wala kondoo wengine hawaamuriwi kufanya hivyo. (Wakolosai 2:16, 17) Hata hivyo, Paulo aliwaambia Wakristo watiwa-mafuta Waebrania hivi: “Kumebaki pumziko la sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana mtu ambaye ameingia ndani ya pumziko la Mungu amepumzika pia mwenyewe kutokana na kazi zake mwenyewe, kama vile Mungu alivyofanya kutokana na zake mwenyewe.” (Waebrania 4:9, 10) Waebrania hao waliingia katika “pumziko la sabato” walipojitiisha kwa “uadilifu wa Mungu” na kupumzika kutoka hali ya kujaribu kujitetea kwa kazi za Sheria. (Waroma 10:3, 4) Wakristo watiwa-mafuta Wasio Wayahudi huonea shangwe pumziko lilelile kwa kujitiisha kwa uadilifu wa Yehova. Umati mkubwa hujiunga nao katika pumziko hilo.
6. Kondoo wengine leo hujiwekaje chini ya agano jipya?
6 Zaidi, kondoo wengine hujiweka chini ya agano jipya kama vile wageni wa zamani walivyojiweka chini ya agano la Sheria. Katika njia gani? Si kwa kuwa washiriki katika hilo bali kwa kujinyenyekeza kwa sheria zinazoshirikishwa nalo na kunufaika kutokana na mipango yake. (Linganisha Yeremia 31:33, 34.) Kama waandamani wao watiwa-mafuta, kondoo wengine wana sheria ya Yehova ikiwa imeandikwa ‘katika moyo wao.’ Wao huzipenda sana na kuzitii amri na kanuni za Yehova. (Zaburi 37:31; 119:97) Kama Wakristo watiwa-mafuta, wao wamjua Yehova. (Yohana 17:3) Vipi juu ya tohara? Miaka ipatayo 1,500 kabla ya kufanywa kwa agano jipya, Musa aliwahimiza Waisraeli hivi: “Zitahirini govi za mioyo yenu.” (Kumbukumbu la Torati 10:16; Yeremia 4:4) Ingawa tohara ya kimwili ya lazima ilipitilia mbali pamoja na Sheria, watiwa-mafuta na pia kondoo wengine lazima ‘watahiri’ mioyo yao. (Wakolosai 2:11) Mwishowe, Yehova husamehe kosa la kondoo wengine kwa msingi wa “damu [ya Yesu] ya agano” iliyomwagwa. (Mathayo 26:28; 1 Yohana 1:9; 2:2) Mungu hawafanyi kuwa wana wa kiroho, kama vile ambavyo huwafanya wale 144,000. Lakini yeye huwatangaza kondoo wengine kuwa waadilifu, katika maana ambayo Abrahamu alitangazwa kuwa mwadilifu akiwa rafiki ya Mungu.—Mathayo 25:46; Waroma 4:2, 3; Yakobo 2:23.
7. Ni tazamio gani liwezekanalo kwa ajili ya kondoo wengine leo, ambao hutangazwa kuwa waadilifu kama vile Abrahamu?
7 Kwa wale 144,000, kutangazwa kuwa waadilifu huwafungulia njia kulikubali tumaini la kutawala na Yesu katika Ufalme wa kimbingu. (Waroma 8:16, 17; Wagalatia 2:16) Kwa kondoo wengine, kutangazwa kuwa waadilifu wakiwa rafiki za Mungu huwawezesha kuwa na tumaini la uhai udumuo milele katika dunia iliyo paradiso—ama kwa kuokoka Har–Magedoni wakiwa sehemu ya umati mkubwa ama kupitia “ufufuo wa waadilifu.” (Matendo 24:15) Ni pendeleo lililoje kuwa na tumaini la namna hiyo na kuwa rafiki ya Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima, kuwa “mgeni-mwalikwa katika hema [lake]”! (Zaburi 15:1, 2, NW) Ndiyo, watiwa-mafuta na kondoo wengine hubarikiwa katika njia ya ajabu kupitia Yesu, Mbegu ya Abrahamu.
-