Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jitihada za Muda Mrefu za Kuboresha Afya
    Amkeni!—2004 | Mei 22
    • Tauni

      Yaonekana kwamba tauni hiyo ilianza mwaka wa 1347, wakati meli kutoka Crimea ilipotia nanga huko Messina, kwenye kisiwa cha Sicily. Mbali na shehena yake ya kawaida, meli hiyo ilileta tauni pia.a Punde si punde, tauni hiyo ikaenea kotekote nchini Italia.

      Mwaka uliofuata Agnolo di Tura, wa Siena, Italia, alisimulia hali yenye kuogofya iliyokumba mji wao: ‘Watu walianza kufa Siena mnamo mwezi wa Mei. Lilikuwa pigo kali lenye kuogofya. Wagonjwa walikufa punde baada ya kuambukizwa. Mamia ya watu walikufa usiku na mchana.’ Aliongezea hivi: ‘Niliwazika watoto wangu watano, na ndivyo walivyofanya wengine wengi pia. Hakuna aliyeomboleza, hata awe alifiwa na nani, kwa kuwa kila mtu alikuwa akitazamia kifo. Watu wengi sana walikufa hivi kwamba wote walidhani mwisho wa dunia umefika.’

      Wanahistoria fulani wanasema kwamba tauni hiyo ilienea kotekote barani Ulaya kwa kipindi cha miaka minne na kwamba thuluthi moja hivi ya watu walikufa, watu kati ya milioni 20 na milioni 30. Hata katika nchi ya mbali ya Iceland watu wengi sana walikufa. Inasemekana kwamba katika Mashariki ya Mbali, idadi ya wakaaji wa China ilishuka kutoka milioni 123 mwanzoni mwa karne ya 13 hadi milioni 65 katika karne ya 14, huenda kutokana na tauni hiyo pamoja na njaa kali iliyozuka wakati huohuo.

      Hakuna ugonjwa mwingine wowote, vita, au njaa kali iliyokuwa imesababisha kuteseka kulikoenea hivyo. “Ulikuwa msiba usio na kifani katika historia ya wanadamu,” chasema kitabu Man and Microbes. “Ugonjwa huo uliangamiza kati ya asilimia 25 na asilimia 50 ya watu barani Ulaya, Afrika Kaskazini, na sehemu mbalimbali za Asia.”

      Mabara ya Amerika hayakupatwa na tauni hiyo kwa sababu yalikuwa mbali na sehemu nyingine za ulimwengu. Hata hivyo, meli zilipoanza kufika huko, magonjwa hayo yakaanza kuenea huko pia. Katika karne ya 16, magonjwa hatari hata kupita tauni yalikumba mabara hayo.

  • Jitihada za Muda Mrefu za Kuboresha Afya
    Amkeni!—2004 | Mei 22
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 6]

      Mambo ya Hakika na Ushirikina

      Katika karne ya 14, wakati ambapo tauni ilikumba nyumba ya papa huko Avignon, daktari wake alimjulisha kwamba mpangilio wa sayari tatu, yaani Zohali, Sumbula, na Mars, uliofanyiza umbo la Aquarius ndio uliosababisha tauni hiyo.

  • Jitihada za Muda Mrefu za Kuboresha Afya
    Amkeni!—2004 | Mei 22
    • [Picha katika ukurasa wa 4]

      Mchongo wa Kijerumani wa mwaka wa 1500 hivi, unaoonyesha daktari ambaye amejifunika kitambaa ili kujikinga na tauni. Sehemu iliyofunika mdomo ina marashi

      [Hisani]

      Godo-Foto

      [Picha katika ukurasa wa 4]

      Bakteria iliyosababisha tauni ya majipu

      [Hisani]

      © Gary Gaugler/Visuals Unlimited

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki