Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2006 la “Ukombozi Unakaribia”
    Huduma ya Ufalme—2005 | Desemba
    • Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2006 la “Ukombozi Unakaribia”

      1 Mfalme Hezekia wa Yuda la kale alitumia wakimbiaji kupeleka barua za kuwaita watu wakusanyike pamoja Yerusalemu. (2 Nya. 30:6, 13) Itikio la watu lilionyesha mtazamo wao kuelekea ibada ya kweli. (2 Nya. 30:10-12) Miezi michache ijayo, watumishi wa Yehova watakuwa na fursa kama hiyo ya kuonyesha uthamini wao wa kutoka moyoni kwa tukio la pekee la kukusanyika pamoja ili kumwabudu Yehova. Barua ya kuwaalika mhudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Ukombozi Unakaribia” imetumwa katika kutaniko lenu. Utaitikiaje mwaliko huo?

      2 Fanya Mipango Sasa: Ili tunufaike kabisa na programu ya kiroho ambayo inatayarishwa, tunahitaji kuhudhuria programu yote. Anza kufanya mipango yoyote inayohitajiwa sasa ili wewe pamoja na familia yako mhudhurie siku zote tatu. (Met. 21:5) Huenda matayarisho hayo yakatia ndani kumwomba mwajiri wako ruhusa, kuzungumzia mipango yako na mwenzi asiyeamini, kufanya mipango ya mahali pa kulala, na kusaidia wanafunzi wa Biblia wahudhurie siku zote. Usiahirishe mambo hayo muhimu hadi dakika ya mwisho. Badala yake, sali kwa Yehova kuhusu mambo hayo, ukitumaini kwamba ‘yeye mwenyewe atatenda.’—Zab. 37:5.

      3 Tengenezo la Yehova limejitahidi ili kuhakikisha kwamba kutakuwa na vyumba vya kulala vya kutosha kwenye kila mji au jiji la kusanyiko. Kuthamini jitihada za ndugu zetu waliofanya kazi kwa bidii ili kusaidia kufanya mipango hiyo, kuwafikiria ndugu na dada wenzetu watakaohudhuria kusanyiko, na kuheshimu utaratibu wa kitheokrasi kunapaswa kutuchochea tufuate kikamili mwongozo ambao umetolewa katika makala hii.—1 Kor. 13:5; 1 The. 5:12, 13; Ebr. 13:17.

  • Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2006 la “Ukombozi Unakaribia”
    Huduma ya Ufalme—2005 | Desemba
    • 11 Mvulana mmoja mwenye umri wa miaka mitano alisema hivi alipokuwa akihudhuria kusanyiko la wilaya: “Kati ya mambo ninayofurahia zaidi katika ibada ya Yehova ni kuhudhuria kusanyiko la wilaya.” Maelezo hayo ya kutoka moyoni hutusaidia sote tutambue furaha ambayo sisi hupata tunapohudhuria kusanyiko la wilaya kila mwaka. Ni kama vile mtunga-zaburi alivyoimba: “Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko.” (Zab. 84:10) Kupitia wimbo, Daudi alionyesha tamaa yake ya ‘kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yake, ili aweze kulitazama kwa uthamini hekalu la Yehova.’ (Zab. 27:4) Daudi alifurahi sana kuwa miongoni mwa waabudu wa Yehova. Na tuonyeshe uthamini kama huo kwa ajili ya ibada ya kweli kwa kuhudhuria siku zote tatu za Kusanyiko la Wilaya la “Ukombozi Unakaribia.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki