-
Familia Kubwa Zilizoungana Katika Utumishi wa MunguMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
Familia ya Uwadiegwu, anayeishi Afrika Magharibi ni mfano mmoja. Ijapokuwa Uwadiegwu na mke wake wana watoto wanane, wote wawili wanatumikia wakiwa mapainia wa kawaida, au wahudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova. Yeye asema: “Familia yetu imedumisha funzo la Biblia la ukawaida kwa zaidi ya miaka 20. Tumefundisha watoto Neno la Mungu tangu walipokuwa watoto wadogo, si wakati wa funzo la familia tu, bali pia katika huduma na nyakati nyinginezo. Watoto wetu wote ni wapiga-mbiu wa habari njema za Ufalme, na yule ambaye hajabatizwa bado ni yule mdogo zaidi tu aliye na umri wa miaka sita.”
-
-
Familia Kubwa Zilizoungana Katika Utumishi wa MunguMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
Kazi ya pamoja hutia ndani kuwapa watoto madaraka ya kiroho wanapokuwa tayari kufanya hivyo. Baba mmoja, mzee Mkristo mwenye watoto 11, huamka asubuhi na mapema ili kuongoza mafunzo na watoto kadhaa kabla ya kwenda kazini. Wale wakubwa, wanapobatizwa, huwasaidia ndugu na dada zao wachanga kwa zamu, hiyo yatia ndani kushiriki katika kuwafundisha Biblia. Baba huwasimamia, akiwapongeza kwa jitihada zao. Sita kati ya watoto hao wamebatizwa, na wengine wanaendelea kujitahidi kufikia mradi huo.
Mawasiliano Mazuri, Miradi ya Pamoja
Lililo muhimu katika familia zilizoungana ni mawasiliano yenye upendo na miradi ya kiroho ya pamoja. Gordon, mzee Mkristo anayeishi Nigeria, ni baba ya watoto saba wenye umri wa kati ya miaka 11 hadi miaka 27. Sita kati yao ni mapainia, kama vile wazazi wao. Yule mdogo zaidi, aliyebatizwa hivi majuzi, hushiriki kwa ukawaida katika kazi ya kufanya wanafunzi na wale wengine katika familia. Wana wawili ambao ni watu wazima ni watumishi wa huduma katika kutaniko.
Gordon aliongoza mwenyewe mafunzo ya Biblia pamoja na kila mmoja wa watoto wake. Mbali na hilo, familia hiyo ina programu yenye mambo mengi ya elimu ya Biblia. Wao hukutana kila asubuhi ili kuchunguza andiko la Biblia kisha kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko.
Mojawapo ya miradi iliyowekwa kwa kila mshiriki wa familia ni kusoma makala zote katika magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Hivi majuzi, waliongezea usomaji wa Biblia wa kila siku katika kawaida yao ya usomaji. Kwa kuzungumzia yale wanayosoma, washiriki wa familia hutiana moyo kuendeleza zoea hilo.
Funzo la Biblia la familia la kila juma limeimarika vizuri sana hivi kwamba hakuna mtu ambaye huhitaji kikumbusha—kila mtu hulitazamia. Kwa miaka kadhaa, mambo yaliyomo, muundo wake, na urefu wa funzo la familia, yametofautiana kulingana na umri na mahitaji ya watoto. Familia hiyo imekuwa na ukaribu pamoja na watumishi wengine waaminifu wa Mungu, na hilo limekuwa na matokeo yenye kunufaisha watoto.
-
-
Familia Kubwa Zilizoungana Katika Utumishi wa MunguMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
Monica, anayeishi Kenya, ni mmoja wa watoto kumi. Yeye asema: “Wazazi wangu walitufunza kweli ya Biblia tangu utotoni. Baba alikuwa akitufunza vichapo vya Kikristo kila juma. Kwa sababu ya kazi yake, funzo halikuwa siku ileile sikuzote. Nyakati nyingine, alipokuwa akirudi nyumbani kutoka kazini, angetuona tukicheza nje na kutuambia kwamba baada ya dakika tano ilitupasa tuingie ndani kwa ajili ya funzo letu la Biblia. Baada ya funzo letu la Biblia, tulikuwa tukitiwa moyo kuuliza maswali na kuzungumzia matatizo yetu.
-