-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Japani
Miho alipokaribia wakati wake wa kujifungua, hakuweza kushiriki katika kazi ya kuhubiri kama kawaida. Kwa sababu alitaka kuendelea na upainia, alimwomba mwangalizi wa utumishi anwani za watu wanaoishi katika ghorofa zenye ulinzi mkali au nyumba nyingine ambamo wahubiri hawawezi kuingia. Alipewa anwani 100 hivi, naye akawapigia simu watu wengi iwezekanavyo. Mara ya kwanza hakuna hata mmoja aliyetaka kusikiliza, na alimaliza kuwapigia wote simu kwa dakika 30 tu. Baadaye, alipiga simu kwanza, kisha akaandika barua. Alipoandika barua alirejelea habari zozote zile alizopata alipopiga simu, kama vile mtoto aliyelia nyumbani kwa yule aliyempigia. Aliruhusu muda kupita ili barua ifike, kisha akapiga simu tena na kuzungumzia faida ya kufuata mwongozo wa Biblia aliokuwa ametaja katika barua. Mwanamke fulani alikataa kuzungumza naye kwa simu, hata hivyo Miho alimtumia barua. Miho alipopiga simu tena, binti yake tu ndiye aliyekuwa nyumbani. Msichana huyo aliye mwanafunzi wa shule alikuwa amesoma barua hiyo. Miho alimhubiria na kumwahidi angemwandikia mashauri ya Biblia yanayoweza kuwasaidia wanafunzi shuleni. Alipanga pia kumpigia simu tena. Mama yake alijibu simu wakati huo na kumwambia Miho kwamba binti yake amekuwa na matatizo shuleni na mashauri ambayo Miho alimpa yamemsaidia. Baada ya kupigiwa simu na kuandikiwa mara kadhaa, mama huyo na binti yake walianza kujifunza.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 43]
Miho
-