-
Hubiri Ili Kufanya WanafunziMnara wa Mlinzi—2003 | Novemba 15
-
-
12-14. Ili kuonyesha manufaa ya mahubiri ya simu, simulia jambo ulilojionea au mojawapo ya mambo yaliyotajwa kwenye mafungu haya.
12 Alipokuwa akihubiri nyumba kwa nyumba huko Brazili, Mkristo tutakayemwita Maria alimpa trakti mwanamke mmoja kijana aliyekuwa anaondoka katika jengo fulani. Maria alitumia kichwa cha trakti hiyo kama utangulizi, na kumwuliza, “Je, ungependa kujua mengi zaidi kuhusu Biblia?” Mwanamke huyo akamjibu: “Ningependa. Lakini tatizo ni kwamba mimi ni mwalimu, na hutumia wakati wangu wote kufundisha.” Maria alimweleza kwamba wangeweza kuzungumzia habari za Biblia kupitia simu. Mwanamke huyo alimpa Maria namba yake ya simu, kisha jioni hiyohiyo akaanza kujifunza broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?a kupitia simu.
-
-
Hubiri Ili Kufanya WanafunziMnara wa Mlinzi—2003 | Novemba 15
-
-
14 Mtangazaji mmoja wa Ufalme huko Denmark ambaye alianzisha funzo la Biblia kwa kuhubiri kupitia simu anasema: “Mwangalizi wa utumishi alinitia moyo nishiriki katika mahubiri ya kutumia simu. Mwanzoni nilisita nikisema: ‘Sipendelei mahubiri hayo.’ Hata hivyo, siku moja nilipiga moyo konde na nikampigia simu mwenye-nyumba wa kwanza. Sonja alijibu simu hiyo, na baada ya mazungumzo mafupi akakubali vichapo vinavyozungumzia Biblia. Jioni moja tulizungumza kuhusu uumbaji, na mwanamke huyo akataka kusoma kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation.b Nilimwambia kwamba ingekuwa vema kama tungekutana uso kwa uso na kuzungumzia habari hiyo. Alikubali. Nilipofika, Sonja alikuwa tayari kujifunza na tangu wakati huo tumekuwa tukijifunza kila juma.” Dada yetu Mkristo anamalizia: “Nilikuwa nimesali kwa miaka mingi ili nipate funzo la Biblia, lakini sikutazamia kupata funzo kupitia mahubiri ya simu.”
-