-
Waazteki wa Kisasa Wajifunza na Kuwa Wakristo wa KweliMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 1
-
-
Mwanamke fulani mwenyeji aliposikia hotuba ya Biblia katika Kinahuatl kwa mara ya kwanza, alisema: “Tumekuwa tukihudhuria mikutano kwa miaka kumi na kurudi nyumbani tukiumwa na kichwa kwa sababu hatukuelewa Kihispania vizuri. Lakini sasa, ni kana kwamba tumeanza maisha upya!” Juan, mwenye umri wa miaka 60 amekuwa akijifunza Biblia na kuhudhuria mikutano ya Kihispania pamoja na mke wake na watoto wao kwa miaka minane bila kufanya maendeleo yoyote. Kisha, akaanza kujifunza Biblia katika Kinahuatl. Katika muda usiozidi mwaka mmoja, alibatizwa na kuwa Shahidi!
-
-
Waazteki wa Kisasa Wajifunza na Kuwa Wakristo wa KweliMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 1
-
-
Katika mji wa San Agustín Oapan, Mashahidi wa Yehova walikatazwa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Kulikuwa na wasiwasi kwamba jambo hilo lingewachochea watu waache kutoa pesa za kulipia sherehe hizo. Wakati Florencio na kikundi kidogo cha Mashahidi Wanahuatl walipokuwa wakihubiri, watatu kati yao walikamatwa. Katika muda wa dakika 20, umati ulikusanyika ili kuamua hatua ambayo wangewachukulia.
“Walitaka kutuua papo hapo,” Florencio anasema. “Baadhi yao walisema tufungwe na kutupwa mtoni ili tufe maji! Tulikaa gerezani usiku mmoja. Siku iliyofuata, Shahidi aliyekuwa wakili na Mashahidi wengine wawili walikuja kutusaidia. Wao pia wakatupwa gerezani. Mwishowe, wenye mamlaka walikubali kutuachilia ikiwa tu tungeondoka katika mji huo.” Licha ya hayo, kutaniko lilianzishwa mwaka mmoja baadaye, likiwa na Mashahidi 17 waliobatizwa na watu 50 hivi walihudhuria mikutano.
Alberto, ambaye ni Shahidi wa Yehova, alikaribishwa kwenye sherehe ya jamii ya Wanahuatl wa Coapala. Alikataa na akatupwa gerezani. Watu wa jamii hiyo walifanya mkutano, na baadhi yao wakapendekeza anyongwe ili kuwatisha watu wengine ambao wangetaka kujiunga na dini yake na kuacha desturi zao. Mashahidi wengine walijaribu kumsaidia ili aachiliwe, lakini wao pia wakakamatwa. Wote waliachiliwa baada ya sherehe hiyo ya juma moja. Upinzani ulipoendelea, Mashahidi walilazimika kutafuta msaada kwa wenye mamlaka ya juu, hivyo, agizo likatolewa la kukomesha mateso hayo. Inapendeza kwamba mwanamume aliyekuwa mpinzani mkuu alikubali kweli ya Biblia na muda si muda, akabatizwa. Sasa kuna kutaniko katika mji huo.
-
-
Waazteki wa Kisasa Wajifunza na Kuwa Wakristo wa KweliMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 1
-
-
Sonia, mhudumu wa wakati wote, anaeleza kilichomchochea ajifunze lugha hiyo. “Kuna wahamiaji 6,000 hivi wanaozungumza Kinahuatl ambao wanaishi karibu na nyumbani kwangu. Wanaishi katika vibanda vyenye ua na walinzi. Watu hao wamefedheheshwa na hawana usalama,” asema Sonia. “Hali zao zilinihuzunisha sana kwa sababu pindi moja walijivunia maisha yao, nao ndio chanzo cha utamaduni wetu. Tulikuwa tumewahubiria kwa Kihispania kwa miaka 20, lakini hawakupendezwa sana wala kuuelewa vizuri ujumbe wetu. Hata hivyo, nilipojifunza maneno machache ya lugha yao, hali ilibadilika. Walikuwa wakinizunguka wakitaka kusikiliza. Nilijitolea kumfundisha mwanamke mmoja kusoma na kuandika kama angenifundisha Kinahuatl. Sasa wananijua kwenye vibanda vyote kuwa ‘mwanamke anayezungumza Kinahuatl.’ Ninahisi kama mmishonari katika nchi yangu.” Sasa kuna kutaniko la Kinahuatl katika eneo hilo.
Maricela, mhudumu mwingine wa wakati wote, anajitahidi kujifunza Kinahuatl. Mwanzoni, alijifunza Biblia akitumia Kihispania na mzee wa miaka 70 aitwaye Félix. Maricela aliendelea kujifunza Kinahuatl, kwa hiyo, akaanza kumfundisha Félix katika lugha yake. Matokeo yalikuwa mazuri. Aliguswa moyo sana wakati Félix alipomuuliza: “Je, Yehova husikiliza ninapozungumza naye katika Kinahuatl?” Félix alifurahi kujua kwamba Yehova anaelewa lugha zote. Sasa Félix amebatizwa na anahudhuria mikutano kwa ukawaida hata ingawa analazimika kutembea kwa miguu kwa muda wa saa moja na nusu ili kufika mikutanoni. Maricela anasema, “Ninafurahi sana kushirikiana na malaika ambaye ana habari njema ya kuwatangazia watu wote!”—Ufunuo 14:6, 7.
-