-
Kitabu cha Hekima Chenye Ujumbe Unaofaa LeoMnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 1
-
-
Je, Unataka kufanikisha Maisha Yako?
Mradi wa watu wengi leo ni kurundika mali. Hata hivyo, mfanya-biashara tajiri wa Marekani ambaye ametoa mamilioni ya dola kwa mashirika ya kusaidia wenye shida alisema hivi wakati mmoja: “Pesa huvutia watu fulani, lakini hakuna awezaye kuvaa jozi mbili za viatu wakati mmoja.” Ni watu wachache wanaokubali uhakika huo, nao wanaoacha kufuatia mali ni wachache hata zaidi.
Hitoshi alikua akiwa maskini, kwa hiyo alikuwa na tamaa kubwa ya kuwa tajiri. Baada ya kuona namna wenye kudai walivyowatumia kwa hila wadeni wao, yeye aliamua hivi: “Yule anyakuaye pesa nyingi zaidi ndiye mshindi.” Hitoshi alikuwa na imani kubwa katika uwezo wa pesa hivi kwamba alifikiri hata uhai wa wanadamu ungeweza kununuliwa kwa pesa. Ili kurundika mali, alifanya biashara yake ya ufundi-bomba kwa bidii, akiifanya mwaka wote, bila kupumzika hata siku moja. Punde si punde, Hitoshi, akiwa mwana-kandarasi msaidizi, aling’amua kwamba hata kama angejitahidi kadiri gani, hangekuwa na uwezo sawa na wenye kandarasi ambao walimwajiri. Kuvunjika moyo na kuhofia kufilisika yakawa mambo aliyolazimika kukabili kila siku.
Ndipo mwanamume fulani akamtembelea Hitoshi na kumwuliza kama alijua kwamba Yesu Kristo alikufa kwa ajili yake. Kwa kuwa Hitoshi alifikiri kwamba hakuna yeyote ambaye angekufa kwa ajili ya mtu kama yeye, alitaka kujua zaidi naye akakubali mazungumzo zaidi. Juma lililofuata, alihudhuria hotuba fulani na kushtuka kusikia onyo juu ya ‘kuweka jicho likiwa sahili.’ Msemaji alieleza kwamba jicho “sahili” ni lile ambalo huzingatia mambo ya baadaye na hukazwa juu ya mambo ya kiroho; ilhali jicho lenye “husuda” hukazwa tu juu ya tamaa za kimwili za wakati huohuo na halizingatii mambo ya baadaye. Shauri, “Mahali ilipo hazina yako, ndipo moyo wako utakapokuwa pia,” lilimgusa moyo.f Kuna jambo fulani lililo muhimu zaidi kuliko kupata mali! Hakuwa amewahi kusikia jambo kama hilo.
Akiwa amevutiwa sana, alianza kufanya yale aliyokuwa akijifunza. Badala ya kuchoka akitafuta pesa, alianza kutanguliza mambo ya kiroho maishani mwake. Pia, alitumia wakati kushughulikia hali njema ya kiroho ya familia yake. Bila shaka, hilo lilimaanisha kwamba angetumia wakati mchache zaidi kazini, hata hivyo, biashara yake ilisitawi. Kwa nini?
Alipoitikia shauri alilopewa, utu wake wenye ugomvi ulibadilika akawa mpole na mwenye amani. Alivutiwa hasa na onyo hili la upole: “Kwa kweli yawekeni mbali nanyi hayo, hasira ya kisasi, hasira, ubaya, usemi wenye kuudhi, na maongezi yenye aibu kutoka katika kinywa chenu. Msiwe mkiambiana uwongo. Uvueni utu wa zamani pamoja na mazoea ya huo, na mjivike wenyewe utu mpya, ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano wa Yule aliyeuumba.”g Kufuata shauri hilo hakukumfanya tajiri, lakini ‘utu wake mpya’ uliwavutia sana wateja wake, wakawa na itibari na uhakika katika yeye. Naam, maneno ya hekima aliyopata yalimsaidia kufanikisha maisha yake. Kwake, maneno hayo yalikuwa yenye thamani kubwa kuliko mfuko uliojaa lulu au pesa.
-
-
Kitabu cha Hekima Chenye Ujumbe Unaofaa LeoMnara wa Mlinzi—1999 | Aprili 1
-
-
Maneno ya Hekima ili Kufanikisha Maisha
“Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA; bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.”—Mithali 11:1.
“Kiburi hutangulia uangamivu; na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.”—Mithali 16:18.
“Asiyetawala roho yake ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.”—Mithali 25:28.
“Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.”—Mhubiri 7:9.
“Tupa chakula chako usoni pa maji; maana utakiona baada ya siku nyingi.”—Mhubiri 11:1.
“Msiache usemi uliooza utoke kinywani mwenu, bali usemi wowote ule ulio mwema kwa ajili ya kujenga kama vile kuwezavyo kuwa na uhitaji, ili huo upate kuwapa wasikiaji lililo la kupendeleka.”—Waefeso 4:29.
-