Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Tupo Hapa?
    Amkeni!—2008 | Desemba
    • Dave alikuwa na kazi yenye mshahara mnono, nyumba nzuri, na alifurahia kuwa pamoja na marafiki wake. Anasema hivi: “Usiku mmoja nilikuwa nikirudi nyumbani kutoka kwenye sherehe nilipojiuliza swali hili, ‘Je, hili ndilo kusudi la uhai?—Je, nitaishi kwa muda mfupi tu kisha nife? Au je, kuna kusudi lingine?’ Jambo lililonisumbua ni kugundua sikuwa na kusudi maishani wakati huo.”

      Katika kitabu chake Man’s Search for Meaning, Viktor Frankl alisema kwamba baada ya kuachiliwa kutoka katika kambi za mateso, baadhi ya waokokaji wenzake wa yale Maangamizi Makubwa waliuliza swali kama hilo. Waliporudi nyumbani, baadhi yao walikuta kwamba wapendwa wao walikuwa wameangamia. Frankl aliandika hivi: “Ole wake yule ambaye siku ya kuachiliwa, alikuta maisha yakiwa tofauti sana kuliko alivyotarajia!”

      Watu Wanaouliza Swali Hilo

      Swali kuhusiana na kusudi la uhai limeulizwa na watu katika vizazi vyote. Biblia inatuambia kuhusu watu waliotaka kujua maisha yana kusudi gani. Ayubu aliuliza hivi baada ya kupoteza mali na watoto wake na alipougua ugonjwa mbaya: “Kwa nini sikufa tokea tumbo la uzazi? Kwa nini sikutoka tumboni kisha nikate pumzi?”—Ayubu 3:11.

      Nabii Eliya alihisi vivyo hivyo. Huku akihisi kwamba yeye ndiye mwabudu pekee wa Mungu, alilalamika hivi: “Inatosha! Sasa, Ee Yehova, iondoe nafsi yangu.” (1 Wafalme 19:4) Watu wengi sana wamehisi hivyo. Kwa kweli, Biblia inamfafanua Eliya kuwa “mtu mwenye hisia kama zetu.”—Yakobo 5:17.

      Safari Yenye Mafanikio Maishani

      Maisha hulinganishwa na safari. Kama vile unavyoweza kuanza safari bila kufikiria utafika wapi, unaweza kuishi bila kutambua kusudi halisi la maisha. Ukifanya hivyo, utakuwa kama watu ambao mwandishi anayejulikana Stephen R. Covey anasema wanatafuta kusudi kwa kufanya maisha yawe yenye shughuli nyingi sana. Aliandika kuhusu wale ambao “wanapata mafanikio yasiyo na maana, mafanikio ambayo wamepata kwa kupoteza vitu ambavyo ghafula wanatambua vilikuwa vya muhimu zaidi kwao.”

      Je, hukubali kwamba kuongeza mwendo katika safari ni bure ikiwa hatuelekei upande unaofaa? Vivyo hivyo, kutafuta kusudi maishani kwa kuwa na shughuli nyingi hakutaleta uradhi wa kweli.

  • Unaweza Kupata Wapi Majibu?
    Amkeni!—2008 | Desemba
    • Uchunguzi mmoja ulionyesha kwamba asilimia 66 hivi ya wale waliohojiwa wanaamini kwamba kanisa na masinagogi mengi hayawasaidii watu kupata kusudi maishani.

      Kwa sababu hiyo, wanatafuta majibu kwingineko, iwe ni kupitia sayansi au falsafa za aina mbalimbali. Kwa nini watu wanaendelea kutafuta majibu, ingawa ni wachache tu wanaoonekana kupata uradhi?

      Tuna Uhitaji wa Kiroho

      Dakt. Kevin S. Seybold anasema kwamba kuna “mwelekeo wa wanadamu ulimwenguni pote wa kuabudu kitu fulani.” Katika miaka ya karibuni wanasayansi kadhaa wamefikia mkataa wa kwamba wanadamu wamezaliwa na mwelekeo wa kutafuta kusudi halisi maishani. Watu fulani wanaamini kwamba chembe za urithi na utendaji wa wanadamu unaonyesha kwamba wanadamu wana uhitaji wa asili wa kuwa na uhusiano na nguvu zisizo za kawaida.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki