-
Siku ya Hukumu Ni Nini?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
Mtume Yohana anafafanua hivi Siku ya Hukumu katika Ufunuo 20:11, 12: “Nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikakimbia kutoka mbele zake, na mahali popote hapakupatikana kwa ajili ya hizo. Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.” Hukumu hiyo itatekelezwa na nani?
Yehova Mungu ndiye Hakimu au Mwamuzi mkuu wa wanadamu. Hata hivyo, ana mwakilishi wa kufanya hukumu. Kulingana na Matendo 17:31, mtume Paulo alisema kwamba Mungu “ameweka siku ambayo katika hiyo anakusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia kwa mwanamume ambaye amemweka rasmi.” Hakimu huyo aliyewekwa rasmi ni Yesu Kristo aliyefufuliwa. (Yohana 5:22)
-
-
Siku ya Hukumu Ni Nini?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
Wakati huo, wale 144,000 watahukumu na kutawala “wakiwa wafalme pamoja na Kristo kwa miaka elfu.” (Ufunuo 14:1-3; 20:1-4; Waroma 8:17) Siku ya Hukumu haitakuwa tukio la haraka la saa 24. Itachukua miaka 1,000.
Katika kipindi hicho cha miaka 1,000, Yesu Kristo ‘atahukumu walio hai na wafu.’ (2 Timotheo 4:1)
-