-
Siku ya Hukumu Ni Nini?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
Mtume Yohana anafafanua hivi Siku ya Hukumu katika Ufunuo 20:11, 12: “Nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikakimbia kutoka mbele zake, na mahali popote hapakupatikana kwa ajili ya hizo. Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.” Hukumu hiyo itatekelezwa na nani?
Yehova Mungu ndiye Hakimu au Mwamuzi mkuu wa wanadamu. Hata hivyo, ana mwakilishi wa kufanya hukumu. Kulingana na Matendo 17:31, mtume Paulo alisema kwamba Mungu “ameweka siku ambayo katika hiyo anakusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia kwa mwanamume ambaye amemweka rasmi.” Hakimu huyo aliyewekwa rasmi ni Yesu Kristo aliyefufuliwa. (Yohana 5:22)
-
-
Siku ya Hukumu Ni Nini?Biblia Inafundisha Nini Hasa?
-
-
Katika kipindi hicho cha miaka 1,000, Yesu Kristo ‘atahukumu walio hai na wafu.’ (2 Timotheo 4:1) “Walio hai” watakuwa “umati mkubwa” utakaookoka Har–Magedoni. (Ufunuo 7:9-17) Mtume Yohana aliwaona pia “wafu . . . wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi” cha hukumu. Kama alivyoahidi Yesu, “waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [Kristo] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Watahukumiwa kwa msingi gani?
Katika njozi, mtume Yohana aliona ‘vitabu vya kukunjwa vikifunguliwa na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.’ Je, vitabu hivyo vya kukunjwa ni rekodi ya mambo ambayo watu walifanya zamani? Hapana, watu hawatahukumiwa kulingana na mambo ambayo walifanya kabla ya kufa. Tunajuaje? Biblia inasema: “Yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake.” (Waroma 6:7) Hivyo, ni kana kwamba wale watakaofufuliwa wataanza upya. Kwa hiyo, vitabu vya kukunjwa vinawakilisha matakwa mengine ya Mungu. Ili waishi milele, wale watakaookoka Har–Magedoni na wale watakaofufuliwa watahitaji kutii amri za Mungu kutia ndani matakwa yoyote mapya ambayo huenda Yehova akafunua katika ile miaka 1,000. Hivyo, watu watahukumiwa kulingana na yale watakayotenda katika Siku ya Hukumu.
-