Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ndoa Ambayo Inanufaisha Mamilioni Wanaoishi Sasa
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Julai 1
    • 14. (a) Ni nani walioandamana na Rebeka? (b) Walikabili safari ya aina gani?

      14 Rebeka alikuwa na waandamani katika safari yake. Kama vile usimulizi unavyoeleza: “Rebeka na mabibi wenye kumtumikia wakainuka na kwenda wakiwapanda ngamia.” (Mwanzo 24:61, NW) Kwa hiyo msafara wa ngamia hao ukafunga safari hatari ya kilometa zaidi ya 800 kupitia eneo la kigeni. “Mwendo wa wastani wa ngamia waliopakiwa mizigo,” kinataarifu kitabu The Living World of Animals, “ni karibu kilometa 4 kwa saa moja.” Ikiwa ngamia za Abrahamu walienda kwa mwendo huo muda wa saa nane kwa siku, ingaliwachukua siku 25 kufika Negebu walikokuwa wakienda.

      15. (a) Tunaona kielelezo gani kizuri sana katika Eliezeri, Rebeka, na wenye kumtumikia? (b) Usimulizi huu unatangulia kuwa kivuli cha nini?

      15 Eliezeri, Rebeka, na mabibi wenye kumtumikia waliutegemea kikamili mwelekezo wa Yehova, hicho kikiwa ni kielelezo kizuri sana kwa Wakristo leo! (Mithali 3:5, 6) Kwa kuongezea, usimulizi huo ni igizo lenye kuimarisha imani. Kama vile tumeona, Abrahamu alikuwa mfananishi wa Yehova Mungu, aliyetoa Mwana wake mpendwa, yule Isaka Mkubwa Zaidi, ili wanadamu wenye dhambi waweze kupata uhai wa milele. (Yohana 3:16) Utayarishaji wa ndoa ya Isaka ulifanywa muda fulani baada ya yeye kuponyoshwa kwenye kifo juu ya madhabahu. Ulikuwa unabii wa utayarishaji wa ndoa ya kimbingu, ambao ulianza kwa bidii baada ya ufufuo wa Yesu.

  • Ndoa Ambayo Inanufaisha Mamilioni Wanaoishi Sasa
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Julai 1
    • 16. (a) Kwa kufaa, mtumishi wa Abrahamu alikuwaje picha ya roho takatifu ya Mungu? (b) Ni swali gani linaloweza kuulizwa kuhusu roho na bibi-arusi?

      16 Jina la Eliezeri linamaanisha “Mungu Wangu Ni Msaidiaji.” Kwa jina na matendo, kwa kufaa yeye ni picha ya roho takatifu ya Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu, ambayo Yeye alipeleka kwenye bara hili la mbali, dunia yetu, ili kuchagua bibi-arusi anayefaa kwa ajili ya Isaka Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo. (Yohana 14:26; 15:26, NW) Jamii ya bibi-arusi ni “lile kundi,” linalojumlika kuwa hivyo kutokana na wanafunzi wa Yesu ambao wamezaliwa kwa roho takatifu wakiwa wana wa kiroho wa Mungu. (Waefeso 5:25-27; Warumi 8:15-17) Sawa na vile Rebeka alivyopokea zawadi za bei kubwa, ndivyo washiriki wa kwanza wa kundi la Kikristo siku ya Pentekoste 33 W.K. walivyopokea zawadi za kimuujiza kuthibitisha wito wao wa kimungu. (Matendo 2:1-4) Kama Rebeka, wao wameyaacha kwa nia mahusiano yote ya kilimwengu na ya kimnofu ili hatimaye waungane pamoja na Bwana-arusi wao wa kimbingu. Kuanzia wakati ambapo washiriki mmoja mmoja wa jamii ya bibi-arusi wanaitwa mpaka kifo chao, ni lazima wao walinde ubikira wao wa kiroho wanapokuwa wakisafiri kupita katika ulimwengu wa Shetani ulio hatari na wenye utongozi. (Yohana 15:18, 19; 2 Wakorintho 11:3; Yakobo 4:4) Ikiwa imejawa na roho takatifu, jamii ya bibi-arusi inawaalika wengine kwa uaminifu washiriki maandalizi ya Yehova kwa ajili ya wokovu. (Ufunuo 22:17) Je! wewe unafuata kielelezo cha bibi-arusi huyo kwa kuuitikia pia mwelekezo wa roho hiyo?

      17. (a) Wale ngamia kumi ni picha ya nini? (b) Mwelekeo wetu unapasa kuwa nini juu ya Biblia na juu ya vichapo vinavyoitegemea Biblia ambavyo vinatayarishwa na jamii ya bibi-arusi? (Matendo 17:11)

      17 Jamii ya bibi-arusi inathamini sana kile ambacho wale ngamia kumi walikuwa picha yacho. Namba kumi inatumiwa katika Biblia kuonyesha ukamilifu au utimilifu kama unavyohusiana na mambo ya duniani. Wale ngamia kumi wanaweza kulinganishwa na Neno la Mungu lililo timilifu na kamilifu, ambalo kupitia hilo jamii ya bibi-arusi inapokea ulishwaji wa kiroho na zawadi za kiroho. (Yohana 17:17; Waefeso 1:13, 14; 1 Yohana 2:5) Ukieleza juu ya tendo la Rebeka la kuwanywesha ngamia, Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 1948 (Kiingereza), ulifanya utumizi huu kuhusu jamii ya bibi-arusi: “Wao wanalifikiria kwa upendo Neno la Mungu ambalo linawapelekea sehemu kubwa ya roho yake. Wanapendezwa na Neno lake lililoandikwa, wakilitumikia na kulitilia burudisho jipya-jipya kwa kulihudumia na kuonyesha hangaikio la moyo mweupe kuhusu ujumbe walo na kusudi lalo, wakitafuta kuliamini.” Kama kielelezo cha jambo hili, mabaki ya jamii ya bibi-arusi yamefanya New World Translation of the Holy Scriptures ya kisasa na yenye burudisho jipya-jipya iweze kupatikana kwa mamilioni ya watu. Iwe au isiwe tafsiri hii nzuri inapatikana katika lugha yako, je! wewe unaonyesha uthamini kwa kuchunguza Biblia kwa ukawaida pamoja na misaada ya kujifunza inayoandaliwa na jamii ya bibi-arusi?​—2 Timotheo 3:16.

      Ndoa ya Mwana-Kondoo Yakaribia

      18. Kwa nini wenye kutumikia Rebeka wanafaa kuwa picha ya waandamani wa bibi-arusi leo?

      18 Katika hizi siku za mwisho za ulimwengu wa Shetani, mabaki ya jamii ya bibi-arusi wameungwa na “umati mkubwa,” unaolinganika na “mabibi wenye kumtumikia’ Rebeka. Kama ilivyokuwa katika kisa cha Rebeka, hawa wanaizidi kwa mbali hesabu ya jamii ya bibi-arusi ya 144,000 iliyo timilifu kitarakimu. Wao ni “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu Kristo. (Ufunuo 7:4, 9; Yohana 10:16, NW) Wakiwa watumikiaji washikamanifu wa bibi-arusi, ni lazima wao pia waendelee bila kuchafuliwa na ulimwengu mwovu wa Shetani. Ni lazima wao pia waitikie miongozo ya roho ya Yehova na Neno lake kama linavyoelezwa kwao na jamii ya bibi-arusi. Lakini thawabu yao ni tofauti. Wakivumilia katika kumuunga mkono bibi-arusi wa Kristo kwa ushikamanifu, wataokoka mwisho wa ulimwengu wa Shetani na kupata fursa nzuri ajabu ya kuishi milele katika Paradiso ya kidunia.​—Ufunuo 21:3, 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki