-
“Ninawezaje Kufanya Ubaya Huu Mkubwa?”Mnara wa Mlinzi—2014 | Novemba 1
-
-
Kijana huyo hakujiruhusu avunjike moyo, alifanya kazi yake kulingana na uwezo wake. Kwa kufanya hivyo alimpa Yehova nafasi ya kumbariki, na Yosefu akapata kibali cha bwana wake mpya. Potifa aliona kwamba mtumishi wake anabarikiwa na Yehova, Mungu wa watu wa Yosefu, na bila shaka baraka hizo zilileta mafanikio makubwa katika nyumba ya Mmisri huyo. Yosefu akazidi kupata heshima machoni pa bwana wake hata Potifa akaviweka vitu vyote mikononi mwa kijana huyo mwenye uwezo.—Mwanzo 39:3-6.
-
-
“Ninawezaje Kufanya Ubaya Huu Mkubwa?”Mnara wa Mlinzi—2014 | Novemba 1
-
-
Simulizi hilo linatuambia kwamba, Yosefu akakua. Akawa mwanamume, “mwenye umbo zuri na sura ya kupendeza.” Maneno hayo yanadokeza hatari iliyokuwa mbele yake, kuwa na sura nzuri mara nyingi huleta uangalifu usiofaa.
Mke wa Potifa alitambua kwamba Yosefu alikuwa mwaminifu
-