-
Kitabu Cha Biblia Namba 1—Mwanzo“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
32. Ni habari gani ya maana iliyo katika Mwanzo juu ya ndoa, nasaba, na kuhesabu wakati?
32 Mwanzo chafunua wazi sana mapenzi na kusudi la Mungu kuhusu ndoa, uhusiano ufaao wa mume na mke, na kanuni za ukichwa na mazoezi ya familia. Yesu mwenyewe alitumia habari hiyo, akinukuu sura ya kwanza na ya pili ya Mwanzo katika ile taarifa moja yake: “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?” (Mt. 19:4, 5; Mwa. 1:27; 2:24) Maandishi katika Mwanzo ni muhimu katika kuonyesha nasaba ya familia ya kibinadamu na pia katika kupiga hesabu ya wakati ambao binadamu amekuwa katika dunia hii.—Mwa., sura 5, 7, 10, 11
-