Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kufaidika na Fadhili-upendo za Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
    • Fadhili-Upendo za Mungu Huleta Kitulizo na Ulinzi

      11, 12. (a) Yehova alimwonyesha Yosefu fadhili-upendo wakati wa majaribu gani? (b) Mungu alimwonyeshaje Yosefu fadhili-upendo?

      11 Sasa, na tuchunguze kitabu cha Mwanzo sura ya 39. Sura hiyo inazungumza juu ya Yosefu, kitukuu wa Abrahamu, ambaye aliuzwa utumwani Misri. Hata hivyo, “BWANA akawa pamoja na [Yosefu].” (Mstari wa 1, 2) Kwa kweli, hata Potifa, Mmisri ambaye alikuwa bwana-mkubwa wa Yosefu, aliona kwamba Yehova alikuwa pamoja na Yosefu. (Mstari wa 3) Hata hivyo, Yosefu alipatwa na jaribu kali sana. Alishtakiwa isivyo kweli kwamba alitaka kumbaka mke wa Potifa na akafungwa gerezani. (Mstari wa 7-20) Akiwa “gerezani,” “walimwumiza miguu yake kwa pingu, akatiwa katika minyororo ya chuma.”—Mwanzo 40:15; Zaburi 105:18.

      12 Ni nini kilichotokea wakati wa jaribu hilo kali sana? “BWANA akawa pamoja na [Yosefu], akamfadhili [“akamwonyesha fadhili-upendo,” NW].” (Mstari wa 21a) Tendo moja hususa la fadhili-upendo lilisababisha mfululizo wa matukio ambayo baadaye yalimletea Yosefu kitulizo kutokana na matatizo yake. Yehova alimwezesha Yosefu kupata “kibali machoni pa mkuu wa gereza.” (Mstari wa 21b) Kwa hiyo, mkuu huyo akampa Yosefu madaraka makubwa. (Mstari wa 22) Halafu, Yosefu akakutana na mtu aliyefanya ajulikane kwa Farao, mtawala wa Misri. (Mwanzo 40:1-4, 9-15; 41:9-14) Baadaye, mfalme alimpandisha Yosefu cheo akawa mtawala wa pili wa Misri. Cheo hicho kilimwezesha kuokoa uhai wakati nchi ya Misri ilipopatwa na njaa kali. (Mwanzo 41:37-55) Mateso ya Yosefu yalianza alipokuwa na umri wa miaka 17 na kuendelea kwa miaka zaidi ya 12! (Mwanzo 37:2, 4; 41:46) Lakini katika miaka hiyo yote ambayo Yosefu aliteseka na kutaabika, Yehova Mungu alimwonyesha fadhili-upendo kwa kumlinda asipatwe na madhara makubwa na kwa kumhifadhi ili kutimiza daraka la pekee katika kusudi la Mungu.

  • Kufaidika na Fadhili-upendo za Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
    • 16. Biblia inatumia maneno gani ya sifa inapozungumza juu ya Abrahamu na Yosefu?

      16 Masimulizi ya kitabu cha Mwanzo sura ya 24 yanaeleza wazi uhusiano wa karibu kati ya Abrahamu na Yehova. Mstari wa kwanza unasema kwamba ‘BWANA alimbariki Abrahamu katika vitu vyote.’ Mtumishi wa Abrahamu alimwita Yehova ‘Mungu wa bwana wangu Abrahamu.’ (Mstari wa 12, 27) Naye mwanafunzi Yakobo anasema kwamba Abrahamu ‘alitangazwa kuwa mwadilifu’ na “akaja kuitwa ‘rafiki ya Yehova.’” (Yakobo 2:21-23) Yosefu pia alikuwa na uhusiano wa karibu na Yehova ambao unakaziwa katika sura yote ya Mwanzo 39. (Mstari wa 2, 3, 21, 23) Zaidi ya hayo, mwanafunzi Stefano alisema hivi kumhusu Yosefu: “Mungu alikuwa pamoja naye.”—Matendo 7:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki