-
Kuhifadi Uhai Katika Wakati wa NjaaMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
1. Ni kitendo gani chenye hekima alichofanya Yusufu wakati wa miaka ile ya utele, na tokeo likawa nini?
MARA tu baada ya kuwekwa kwake rasmi awe Msimamizi wa chakula, Yusufu alitalii nchi ya Misri. Aliagiza mambo yatengenezwe vizuri kufikia wakati miaka ya utele ilianza. Sasa nchi ilizaa mazao tele! Yusufu aliendelea kukusanya vyakula kutoka shamba lililouzunguka kila mji, akiviweka akibani katika mji. Aliendeiea ‘kukusanya nafaka kama mchanga wa pwani, nyingi mno, hata akaacha kuihesabu, maana ilikuwa haina hesabu.’—Mwanzo 41:46-49.
-
-
Kuhifadi Uhai Katika Wakati wa NjaaMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
4. Uandalizi uanofanywa na jamii ya “mtumwa” leo unalinganaje na ule uliotengenezwa katika siku za Yusufu?
4 Mabaki yenye uaminifu ya jamii ya “mtumwa mwenye akili” huyo wanajitahidi Ki-maandiko vyo vyote wawezavyo wahakikishe kwamba Mashahidi walio wakfu wa Yehova, na pia watu wenye kupendeza walioko nje ulimwenguni, wanapokea chakula cha kiroho kinachoendeleza uhai. Amana hiyo inatambuliwa kuwa wajibu mtakatifu na inafanywa kama utumishi mtakatifu kwa Yehova. Tena, “mtumwa” huyo ametengeneza makundi na akayatolea vitabu vya Kibiblia kwa wingi hivi kwamba yana “mbegu” ya kutosha, ya Ufalme ya kutawanya peupe katika mashamba waliyogawiwa. Jambo hilo linalingana na siku za Yusufu, wakati yeye alipowakusanya watu ndani ya miji na kuwaandalia nafaka si kwa ajili ya kujiendeleza wenyewe tu bali pia kwa ajili ya kupanda wakifikiria mavuno ya baadaye.—Mwanzo 47:21-25; Marko 4:14, 20; Mathayo 28:19, 20.
5. (a) Ni fikira gani za pekee ambazo “mtumwa” anaelekeza kwa mahitaji ya watu wa nyumba katika wakati wa shida kubwa? (b) “Mfuriko” wa maandalizi ya kiroho katika 1986 unalingana kwa kadiri gani na yaliyotolewa kule nyuma katika wakati wa Yusufu?
5 Hata wakati kazi ya kuhubiri peupe inapokuwa chini ya marufuku na Mashahidi wa Yehova wanateswa, ‘mtumwa mwaminifu’ anauona uandaaji huo wa chakula cha kiroho kuwa amana takatifu. (Matendo 5:29, 41, 42; 14:19-22) Wakati maafa yanapokumba, kama vile dhoruba, gharika, na matetemeko ya dunia, “mtumwa” anahakikisha kwamba mahitaji ya kimwili na kiroho pia ya watu wa nyumba ya Mungu yanatolewa. Hata wale walio katika kambi za mateso wamefikiwa kwa ukawaida na neno lililopigwa chapa. Mipaka ya taifa hairuhusiwi ikomeshe mtiririko wa chakula cha kiroho kwa wale wanaokihitaji. Kuendelea kutoa chakula hicho bila kuchelewa kunataka ushujaa, imani katika Yehova, na mara nyingi kutumia akili nyingi. Ulimwenguni pote wakati wa 1986 tu, “mtumwa” alitokeza mfuriko wa Biblia na vitabu vyenye majalada magumu 43,958,303, na pia magazeti 550,216,455—kweli kweli kiasi kilicho ‘kingi mno kama mchanga wa pwani.’
-