-
Pumziko la Mungu Ni Nini?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
1, 2. Tunaweza kujifunza nini kutokana na tafsiri sahihi ya andiko la Mwanzo 2:3, na ni maswali gani yanayotokea?
KUANZIA sura ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo, tunajifunza kwamba kwa muda wa siku sita, Mungu aliitayarisha dunia ili iwe makao ya wanadamu. Hizo hazikuwa siku za saa 24 kila moja, vilikuwa vipindi virefu zaidi vya wakati. Biblia inasema hivi kuhusu mwisho wa kila kipindi: “Ikawa jioni, ikawa asubuhi.” (Mwa. 1:5, 8, 13, 19, 23, 31) Hata hivyo, kuhusu siku ya saba, Biblia inasema: “Mungu akaibariki siku ya saba na kuifanya takatifu, kwa kuwa katika siku hiyo amekuwa akipumzika kutokana na kazi yake yote ya kuumba.”—Mwa. 2:3.
2 Kitabu cha Mwanzo kiliposema kwamba Mungu “amekuwa akipumzika,” kilimaanisha kwamba Mungu alikuwa bado anapumzika wakati huo. Hilo linaonyesha kwamba Musa alipoandika kitabu cha Mwanzo mwaka wa 1513 K.W.K. “siku” hiyo ya saba ya Mungu ya kupumzika ilikuwa bado inaendelea. Je, siku ya pumziko la Mungu bado inaendelea? Ikiwa ndivyo, je, tunaweza kuingia katika pumziko hilo leo? Majibu ya maswali au maulizo hayo ni ya maana sana kwetu.
-
-
Pumziko la Mungu Ni Nini?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
5. Ni nini lililokuwa kusudi la siku ya saba, na kusudi hilo litatimia kabisa wakati gani?
5 Ili kujibu swali hilo, ni lazima tukumbuke kusudi la siku ya saba. Andiko la Mwanzo 2:3 linaeleza hivi: “Mungu akaibariki siku ya saba na kuifanya takatifu.” Siku hiyo ‘ilifanywa kuwa takatifu,’ yaani, ilitakaswa, au iliwekwa kando na Yehova ili kukamilisha kusudi lake. Kusudi hilo ni kwamba dunia ikaliwe na wanaume na wanawake watiifu ambao wataitunza na kutunza viumbe wote walio hai. (Mwa. 1:28) Yehova Mungu na Yesu Kristo, ambaye ni “Bwana wa Sabato,” ‘wameendelea kufanya kazi mpaka sasa’ ili watimize kusudi hilo. (Mt. 12:8) Siku ya pumziko la Mungu itaendelea mpaka kusudi lake kuhusiana na siku hiyo litimie kabisa mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo.
-