-
Adui wa Mwisho, Kifo, AangamizwaMnara wa Mlinzi—2014 | Septemba 15
-
-
3, 4. (a) Mungu aliwapa Adamu na Hawa amri gani? (b) Kwa nini ilikuwa muhimu sana kutii amri hiyo?
3 Ingawa Adamu na Hawa walikuwa na tumaini la kuishi milele, hawakuwa na uhai usioweza kufa. Ili waendelee kuishi, ilikuwa lazima wanywe, wale chakula, walale, na kupumua hewa. Jambo muhimu zaidi ni kwamba uhai wao ulitegemea uhusiano wao na Mpaji-Uhai wao. (Kum. 8:3) Ili waendelee kufurahia maisha, walipaswa kukubali mwongozo wa Mungu. Yehova alimwambia Adamu jambo hilo waziwazi hata kabla ya kumuumba Hawa. Alimwambia nini? “Pia Yehova Mungu akamwekea mtu amri hii: ‘Matunda ya kila mti wa bustani unaweza kula mpaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.’”—Mwa. 2:16, 17.
4 “Mti wa ujuzi wa mema na mabaya” uliwakilisha haki ya Mungu ya kuwaamulia yaliyo mema na mabaya. Bila shaka, tayari Adamu alikuwa na uwezo wa kujua mema na mabaya kwa sababu alikuwa na dhamiri na aliumbwa kwa mfano wa Mungu. Mti huo uliwakumbusha Adamu na Hawa kwamba walihitaji mwongozo wa Yehova sikuzote. Kula matunda ya mti huo kungeonyesha kwamba wanataka kuwa na uhuru wa kujiamulia mambo, na hivyo wao na wazao wao wangepata madhara makubwa sana. Amri ya Mungu na adhabu aliyotaja ilionyesha matokeo mabaya sana ya kufanya hivyo.
-
-
Adui wa Mwisho, Kifo, AangamizwaMnara wa Mlinzi—2014 | Septemba 15
-
-
7 Mungu alikuwa amemwambia Adamu hivi: “Siku utakapokula [matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya], utakufa hakika.” Huenda Adamu alielewa kwamba “siku” hiyo ingekuwa ya saa 24. Baada ya kuasi amri ya Mungu, huenda alitarajia Yehova angewachukulia hatua kabla ya jua kutua. Yehova aliwafikia wenzi hao “wakati wenye upepo mtulivu wa siku.” (Mwa. 3:8) Alitenda kama hakimu mahakamani kwa kusikiliza majibu ya Adamu na Hawa ili athibitishe ukweli wa mambo. (Mwa. 3:9-13) Kisha akatangaza hukumu juu ya wakosaji hao. (Mwa. 3:14-19) Kama angewaangamiza papo hapo, kusudi lake kuhusu Adamu na Hawa na wazao wao halingetimia. (Isa. 55:11) Ingawa aliwahakikishia kwamba wangekufa, na wakaanza kuathiriwa na dhambi mara moja, aliwaruhusu Adamu na Hawa wazae watoto ambao wangenufaika na maandalizi mengine kutoka Kwake. Kwa hiyo, machoni pa Mungu, Adamu na Hawa walikufa siku ileile waliyotenda dhambi kwa kuwa miaka 1,000 ni kama “siku” moja kwa Yehova.—2 Pet. 3:8.
-