Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Akusudia Kwamba Mwanadamu Aone Shangwe ya Maisha Katika Paradiso
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Agosti 1
    • 12. Ni lazima Adamu awe alimshukuru Muumba wake kwa jambo gani, na ni jinsi gani mwanadamu angeweza kumtukuza Mungu hivyo?

      12 Ni lazima Adamu awe alimpigia asante Muumba wake kwa kupewa jambo la kumshughulisha kwa njia yenye mafaa katika bustani hii nzuri ya Edeni. Sasa alijua penzi la Muumba wake, na angeweza kumfanyia Yeye jambo fulani duniani. Sasa daraka fulani lilimkalia, lile la kusitawisha bustani ya Edeni na kuitunza, lakini hilo lingekuwa jambo lenye ufurahishi. Kwa kufanya hivi, angeweza kuiendeleza bustani ya Edeni ikiwa na sura yenye kumletea utukufu na sifa Mfanyi wayo, Yehova Mungu. Wakati wowote Adamu alipohisi njaa kwa kufanya kazi, angeweza kula mpaka ashibe kutokana na miti ya bustani. Kwa njia hii angeweza kurudiwa na nguvu zake na kuendeleza maisha yake ya furaha kwa wakati usiojulikana—usio na mwisho.—Linganisha Mhubiri 3:10-13.

  • Mungu Akusudia Kwamba Mwanadamu Aone Shangwe ya Maisha Katika Paradiso
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Agosti 1
    • 14. Ni jinsi gani Adamu angaliweza kuwa na uhai wa milele katika Paradiso?

      14 Uhai wa milele katika bustani ya Paradiso ya Edeni uliwekwa mbele ya Adamu! Ungeweza kuonewa shangwe milele, maadamu yeye angebaki akiwa mtiifu kwa Muumba wake, asile kamwe tunda lililokatazwa na Muumba wa mwanadamu. Tamaa Yake ilikuwa kwamba mwanadamu abaki akiwa mtiifu na kuendelea kuishi milele. Kukataza tunda la “mti wa ujuzi wa mema na mabaya” hakukuwa jambo la kufisha. Ulikuwa mtihani tu wa utii mkamilifu wa mwanadamu kwa Baba yake. Ulimwandalia mwanadamu fursa ya kuthibitisha upendo wake kwa Mungu, Muumba wake.

      15. Kwa nini Adamu angeweza kutazamia kuwa na wakati ujao ulio mwangavu, akipata wema kutoka kwa Muumba wake?

      15 Mwanadamu huyo mkamilifu alitazama mbele katika wakati ujao mwangavu akiwa ametosheka moyoni kwamba yeye hakutokea kiaksidenti tu bila kukusudiwa bali alikuwa na Baba wa kimbingu, akiwa na akili iliyoangaziwa nuru ya kuelewa kusudi lake maishani, akiwa na tazamio la uhai wa milele katika Paradiso. Yeye alikula kutokana na miti iliyokuwa mizuri kwa chakula, akaepuka “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Alitaka kujulishwa mema na Muumba wake. Kazi, ya aina isiyo ya uharibifu, bali ya kusitawisha bustani ya Edeni ilikuwa njema, na mwanadamu huyo mkamilifu alifanya kazi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki