-
Twaweza Kujifunza Kutokana na Wenzi Wawili wa Kwanza wa KibinadamuMnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
MUNGU alikagua sayari Dunia. Alikuwa akiitayarisha ili iwe makao ya wanadamu. Akaona kila kitu alichoumba ni chema. Kwa kweli, alipomaliza kazi hiyo, alisema kwamba ni ‘njema sana.’ (Mwanzo 1:12, 18, 21, 25, 31) Hata hivyo, kabla ya kufikia uamuzi huo mkamilifu Mungu alitaja jambo fulani ambalo ‘halikuwa jema.’ Bila shaka, Mungu hakuumba chochote kisichokuwa kikamilifu. Ni kwamba tu uumbaji wake haukuwa umemalizika bado. “Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye,” Yehova akasema.—Mwanzo 2:18.
-
-
Twaweza Kujifunza Kutokana na Wenzi Wawili wa Kwanza wa KibinadamuMnara wa Mlinzi—2000 | Novemba 15
-
-
Mwanamume alihitaji “msaidizi.” Sasa alikuwa na mmoja ambaye alimfaa kabisa. Hawa alifaa kabisa kuwa msaidizi wa Adamu—katika kutunza makao yao ya bustani na wanyama, kuzaa watoto, na kuwa mwenzi wa kweli aliyemchangamsha kiakili na kumsaidia.—Mwanzo 1:26-30.
-