-
Matazamio Mazuri Ajabu ya Kibinadamu Katika Paradiso Yenye UfurahishiMnara wa Mlinzi—1989 | Agosti 1
-
-
2 “Sasa Yehova Mungu alikuwa akifanyiza kutoka chini kila hayawani-mwitu wa uwanda na kila kiumbe anayeruka wa mbingu, na yeye akaanza kuwaleta kwa mwanadamu aone angemwita nini kila mmoja; na lolote lile ambalo mwanadamu angemwita, kila nafsi aliye hai, hilo lilikuwa ndilo jina lake. Kwa hiyo mwanadamu alikuwa anaita majina ya wanyama wote wa kufugwa na ya viumbe wanaoruka wa mbingu na ya kila hayawani-mwitu wa uwanda.”—Mwanzo 2:19, 20, NW.
3. Kwa nini hakukuwa na hofu kwa upande wa Adamu na viumbe wanyama?
3 Mwanadamu huyo alimwita farasi sus, ng’ombe ndume akamwita shohr, kondoo akamwita seh, mbuzi akamwita ʽez ndege akamwita ʽohph, njiwa akamwita yoh·nahʹ, tausi akamwita tuk·kiʹ, simba akamwita ʼar·yehʹaau ʼariʹa dubu akamwita dov, sokwe akamwita qohph, mbwa akamwita keʹlev, nyoka akamwita na·chashʹ, na kadhalika.a Alipoenda kwenye mto uliotiririka kutoka bustani ya Edeni, aliwaona samaki. Aliwapa samaki jina da·gahʹ. Mwanadamu huyo asiye na silaha hakuhisi akiwahofu wanyama hawa, wa kufugwa na wa mwituni, wala hakuwahofu ndege, nao hawakuhisi wakimhofu yeye, ambaye kwa silika walimtambua kuwa ndiye mkubwa wao, wa aina ya maisha yaliyo ya juu zaidi. Wao walikuwa viumbe wa Mungu, waliopewa na Yeye zawadi ya uhai, na mwanadamu hakuwa na tamaa wala mwelekeo wa kutaka kuwaumiza wala kuwaondolea uhai wao.
4. Tungeweza kufikiri nini kuhusu Adamu alivyowapa majina wanyama na ndege wote, na ni lazima hili liwe lilikuwa tukio la aina gani?
4 Usimulizi hautuambii ni kwa muda gani hasa mwanadamu alikuwa akionyeshwa wanyama wa kufugwa na wa mwituni na viumbe wanaoruka wa mbingu. Yote hayo yalifanywa chini ya mwongozo na mpango wa kimungu. Yaelekea kwamba Adamu alichukua wakati wa kuchunguza kila mnyama tofauti, akiangalia-angalia tabia zake na umbo lake la kumpambanua na wengine; ndipo angechagua jina ambalo lingemfaa huyo sawasawa. Hii ingeweza kumaanisha kwamba muda mwingi vya kutosha ulipita. Lilikuwa tukio la kumpendeza sana Adamu kuzoeana hivyo na viumbe hai wa dunia hii walio wa aina nyingi, naye alihitaji kuwa na uwezo mkubwa wa kiakili na nguvu za uneni ndipo aweze kupambanua kila moja ya aina hizi za viumbe walio hai kwa kuipa jina lililofaa.
-
-
Matazamio Mazuri Ajabu ya Kibinadamu Katika Paradiso Yenye UfurahishiMnara wa Mlinzi—1989 | Agosti 1
-
-
7 Adamu angeshukuru sana kwa usimulizi huo wenye kusisimua juu ya uumbaji. Ulieleza mambo mengi. Kutokana na jinsi ilivyosemwa, yeye alielewa kwamba vilikuwako vipindi virefu vitatu ambavyo Mungu aliviita siku kulingana na njia Yake ya kupima wakati, kabla ya kile kipindi cha nne cha uumbaji ambamo Mungu alitokeza vimulikaji vikubwa viwili katika utandao wa mbingu ili viwe alama ya siku fupi zaidi ya mwanadamu iliyo ya saa 24. Siku hii fupi zaidi ya kibinadamu duniani ilianza wakati wa kushuka kwa kile kimulikaji kikubwa zaidi hadi kushuka kwacho tena. Adamu pia alipata kujua kwamba yeye angekuwa na miaka ya wakati, na bila shaka alianza mara iyo hiyo kuhesabu miaka ya maisha yake. Kimulikaji kilicho kikubwa zaidi katika utandao wa mbingu kingemwezesha kufanya hivyo. Lakini kwa habari ya zile siku ndefu zaidi za uumbaji wa Mungu, mwanadamu wa kwanza aling’amua kwamba wakati huo yeye alikuwa akiishi katika siku ya sita ya kazi ya uumbaji wa kidunia wa Mungu. Hakuna mwisho uliokuwa umekwisha tajwa wa siku hiyo ya sita ya kuumba wanyama wote hao wa bara halafu ya kuumba mwanadamu akiwa kando peke yake. Sasa yeye angeuelewa utaratibu uliofuatwa kuumba mboga hai za kimajani, viumbe hai wa baharini, ndege walio hai, na wanyama wa bara. Lakini akiwa peke yake katika bustani ya Edeni, Adamu hakuwa wonyesho kamili, ulio mtimilifu wa kusudi la Mungu lenye upendo la kufanya mwanadamu awe katika Paradiso yake ya kidunia.
Kuumba Mwanamke wa Kwanza wa Kibinadamu
8, 9. (a) Mwanadamu mkamilifu alichungua akaona nini kuhusu viumbe wanyama, lakini yeye alikata shauri gani kuhusu yeye mwenyewe? (b) Kwa nini ilifaa kwamba mwanadamu mkamilifu hakumwomba Mungu mwenzi? (c) Usimulizi wa Biblia waelezaje juu ya kuumbwa kwa mke wa kwanza wa kibinadamu?
8 Mwanadamu huyo wa kwanza, akiwa na akili yake kamilifu na nguvu za kuchungua mambo, aliona kwamba katika makao ya ndege na wanyama, walikuwamo wa kiume na wa kike na kwamba walizaana kwa aina zao. Lakini kwa habari ya mwanadamu mwenyewe, mambo hayakuwa hivyo wakati huo. Ikiwa maoni ya mchunguo huu yalimwelekeza awe na wazo la kuona shangwe akiwa na mwandamani fulani, yeye hakupata mwenzi anayefaa miongoni mwa yeyote wa wanyama wale, wala hata miongoni mwa masokwe. Adamu angekata shauri kwamba hakukuwa na mwenzi wa kumfaa yeye kwa sababu kama angalikuwako, je! kwani Mungu asingalimletea yeye mwenzi huyo? Mwanadamu alikuwa ameumbwa peke yake kando na aina zote hizo za wanyama, na alikusudiwa awe tofauti! Yeye hakuwa na mwelekeo wa kujiamulia mambo mwenyewe na kukosa busara na kumwomba Mungu Muumba wake ampe mwenzi. Ilifaa mwanadamu huyo mkamilifu aache yote hayo mikononi mwa Mungu, kwa maana muda mfupi baadaye alikuta kwamba Mungu alikuwa amekata mashauri Yake mwenyewe kuhusu hali hiyo. Kuhusu hilo na lile ambalo sasa lilitukia, usimulizi watuambia hivi:
9 “Lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye [kuwa kikamilishio chake, NW]. Bwana [Yehova, NW] Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana [Yehova, NW] Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.”—Mwanzo 2:20-25.
-