-
Kitabu Chenye Kutumika Kwa Maisha Ya KisasaKitabu kwa Ajili ya Watu Wote
-
-
Kinyume cha hilo, Biblia hutoa shauri lenye kutegemeka na lenye usawaziko kwa habari ya ndoa. Inakiri kwamba hali fulani za kupita kiasi hufanya talaka iruhusike. (Mathayo 19:9) Wakati uo huo, inalaumu kutaliki kwa sababu zisizo za maana. (Malaki 2:14-16) Inalaumu pia ukosefu wa uaminifu katika ndoa. (Waebrania 13:4) Inasema kwamba ndoa huhusisha kujifunga wajibu: ‘Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.’a—Mwanzo 2:24; Mathayo 19:5, 6.
-
-
Kitabu Chenye Kutumika Kwa Maisha Ya KisasaKitabu kwa Ajili ya Watu Wote
-
-
a Neno la Kiebrania da·vaqʹ, linalotafsiriwa hapa ‘-shikamana,’ “latia ndani maana ya kuambatana na mtu fulani katika shauku na uaminifu-mshikamanifu.”4 Katika Kigiriki, neno linalofasiriwa “atashikamana” kwenye Mathayo 19:5 linahusiana na neno linalomaanisha “kuunga kwa gundi,” “kuunga kwa saruji,” “kuunganisha pamoja ndindindi.”5
-