-
Kwa Nini Mungu Anaruhusu Watu Wateseke?Mnara wa Mlinzi—2014 | Januari 1
-
-
Sophia: Sawa. “Basi nyoka alikuwa mwenye kujihadhari kuliko wanyama wote wa mwituni ambao Yehova Mungu alikuwa amewafanya. Kwa hiyo akaanza kumwambia mwanamke: ‘Je, ni kweli kwamba Mungu alisema msile matunda ya kila mti wa bustani?’ Mwanamke akamjibu na kumwambia nyoka: ‘Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini kuhusu kula matunda ya mti ulio katikati ya bustani, Mungu amesema, “Msiyale, wala msiyaguse ili msife.”’ Ndipo nyoka akamwambia mwanamke: ‘Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.’”
-
-
Kwa Nini Mungu Anaruhusu Watu Wateseke?Mnara wa Mlinzi—2014 | Januari 1
-
-
Michelle: Kweli kabisa. Ona sasa madai yasiyo ya kweli ambayo Shetani alitoa kumhusu Mungu. Alisema: “Hakika hamtakufa.” Shetani alikuwa akidai kwamba Mungu ni mwongo!
Sophia: Sijawahi kusikia jambo hilo.
Michelle: Shetani alipodai kwamba Mungu ni mwongo, alitokeza suala ambalo lingehitaji wakati ili kutatuliwa. Unajua ni kwa nini?
Sophia: Aaah, sijui.
Michelle: Labda nitumie mfano kuelezea jambo hilo. Tuseme siku moja ninakuja kwako na kudai kwamba nina nguvu kuliko wewe. Ungethibitishaje hilo si kweli?
Sophia: Ningekupa mtihani.
Michelle: Kweli kabisa. Labda tungetafuta chombo kizito na kuona ni nani kati yetu anayeweza kukiinua.Kwa kweli ni rahisi kuthibitisha ni nani aliye na nguvu kuliko mwingine.
Sophia: Ninaelewa unachomaanisha.
Michelle: Lakini namna gani ikiwa badala ya kusema nina nguvu, nidai kwamba mimi ni mnyoofu na wewe si mnyoofu? Hilo ni jambo ngumu kuthibitisha, sivyo?
Sophia: Ndiyo.
Michelle: Kwa kweli, tofauti na nguvu, unyoofu si jambo linaloweza kuthibitishwa kwa urahisi.
Sophia: Ni kweli.
Michelle: Bila shaka, njia rahisi ya kusuluhisha hilo ingekuwa kuacha wakati upite ili wengine wajionee ni nani kati yetu aliye mnyoofu.
Sophia: Umesema kweli.
Michelle: Sasa, angalia tena simulizi hili katika kitabu cha Mwanzo. Je, Shetani alidai kwamba ana nguvu kuliko Mungu?
Sophia: La.
Michelle: Mungu angethibitisha jambo hilo haraka. Lakini Shetani alidai kwamba ni mnyoofu na Mungu si mnyoofu. Ni kana kwamba alimwambia Hawa, ‘Mungu anawadanganya, lakini mimi ninakuambia ukweli.’
Sophia: Hilo linashangaza.
Michelle: Kwa hekima, Mungu alijua kwamba njia bora ya kusuluhisha dai hilo ni kuacha wakati upite. Mwishowe, ingejulikana ni nani aliyesema ukweli na ni nani aliyesema uwongo.
-