Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Uovu Unaendelea
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
    • Biblia inatuambia kile kilichotukia. Shetani Ibilisi alimfikia Hawa na kumwambia hivi kupitia nyoka: “Je, ni kweli kwamba Mungu alisema msile matunda ya kila mti wa bustani?” Hawa aliporudia kutaja amri ya Mungu, Shetani akamwambia hivi: “Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” Basi, Hawa akaona mti huo kuwa wenye kutamanika hivi kwamba “akaanza kuchukua kati ya matunda yake akala.” Masimulizi hayo yanaendelea hivi: “Baadaye akampa mume wake pia alipokuwa pamoja naye, naye akaanza kula.” (Mwanzo 3:1-6) Kwa hiyo, Adamu na Hawa walitumia vibaya uhuru wao wa kuchagua nao wakatenda dhambi kwa kutomtii Mungu.

      Je, unaona uzito wa yale yaliyotukia? Ibilisi alipinga yale ambayo Mungu alikuwa amemwambia Adamu. Maneno ya Shetani yalimaanisha kwamba Adamu na Hawa hawangemhitaji Yehova awaamulie yaliyo mema na yaliyo mabaya. Kwa hiyo, suala ambalo Shetani alitokeza lilitilia shaka haki na uhalali wa utawala wa Yehova juu ya mwanadamu. Basi, suala muhimu sana ambalo Shetani alitokeza lilihusu haki ya Yehova ya kuwa mwenye enzi kuu. Mungu wa kweli alijibu suala hilo jinsi gani?

  • Kwa Nini Uovu Unaendelea
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
    • Miaka 6,000 hivi imepita tangu Shetani alipotilia shaka haki ya Mungu ya kutawala. Historia imefunua nini? Fikiria madai mawili ya Shetani kumhusu Mungu. Shetani alimwambia Hawa kwa ujasiri hivi: “Hakika hamtakufa.” (Mwanzo 3:4) Kwa kusema kwamba Adamu na Hawa hawangekufa ikiwa wangekula tunda lililokatazwa, kwa kweli, Shetani alikuwa akimwita Yehova mwongo. Hilo ni shtaka zito sana! Ikiwa Mungu hakusema kweli katika jambo hilo, angeweza jinsi gani kuaminiwa katika jambo lingine lolote? Hata hivyo, wakati umeonyesha nini?

      Adamu na Hawa walipata magonjwa, maumivu, walizeeka, na mwishowe wakafa. Biblia inasema hivi: “Siku zote ambazo Adamu aliishi zikajumlika kuwa miaka 930, naye akafa.” (Mwanzo 3:19; 5:5) Wanadamu wote wamerithi matokeo hayo yenye kuhuzunisha kutoka kwa Adamu. (Waroma 5:12) Kupita kwa wakati kumethibitisha kwamba Shetani ni “mwongo na ndiye baba ya uwongo” na kumeonyesha kwamba Yehova ni “Mungu wa ukweli.”—Yohana 8:44; Zaburi 31:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki