-
Kwa Nini Uovu UnaendeleaMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Biblia inatuambia kile kilichotukia. Shetani Ibilisi alimfikia Hawa na kumwambia hivi kupitia nyoka: “Je, ni kweli kwamba Mungu alisema msile matunda ya kila mti wa bustani?” Hawa aliporudia kutaja amri ya Mungu, Shetani akamwambia hivi: “Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake macho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” Basi, Hawa akaona mti huo kuwa wenye kutamanika hivi kwamba “akaanza kuchukua kati ya matunda yake akala.” Masimulizi hayo yanaendelea hivi: “Baadaye akampa mume wake pia alipokuwa pamoja naye, naye akaanza kula.” (Mwanzo 3:1-6) Kwa hiyo, Adamu na Hawa walitumia vibaya uhuru wao wa kuchagua nao wakatenda dhambi kwa kutomtii Mungu.
Je, unaona uzito wa yale yaliyotukia? Ibilisi alipinga yale ambayo Mungu alikuwa amemwambia Adamu. Maneno ya Shetani yalimaanisha kwamba Adamu na Hawa hawangemhitaji Yehova awaamulie yaliyo mema na yaliyo mabaya. Kwa hiyo, suala ambalo Shetani alitokeza lilitilia shaka haki na uhalali wa utawala wa Yehova juu ya mwanadamu. Basi, suala muhimu sana ambalo Shetani alitokeza lilihusu haki ya Yehova ya kuwa mwenye enzi kuu. Mungu wa kweli alijibu suala hilo jinsi gani?
-
-
Kwa Nini Uovu UnaendeleaMnara wa Mlinzi—2007 | Septemba 15
-
-
Shetani alimwambia Hawa hivi pia: “Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yake [mti uliokatazwa] macho yenu [ya Hawa na Adamu] yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” (Mwanzo 3:5) Kwa maneno hayo ya ujanja, Shetani aliwadanganya wanadamu kwamba wanaweza kujiongoza. Kwa udanganyifu, Shetani alidokeza kwamba wanadamu wangekuwa na maisha mazuri bila kumtegemea Mungu. Je, hilo limethibitika kuwa kweli?
Katika historia yote, milki mbalimbali zimetokea na kutoweka. Wanadamu wamejaribu serikali za kila aina. Hata hivyo, familia ya wanadamu imekumbwa tena na tena na mambo yenye kuogopesha. Kwa hekima, mwandishi mmoja wa Biblia alikata kauli hii miaka 3,000 hivi iliyopita: “Mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Nabii Yeremia aliandika hivi: “Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Hata maendeleo ya kisayansi na ya kiteknolojia ya miaka ya karibuni hayajapinga ukweli wa maneno hayo. Kupita kwa wakati kumethibitisha tu kwamba maneno hayo ni ya kweli.
-