-
Ufundishaji wa Kimungu Dhidi ya Mafundisho ya MashetaniMnara wa Mlinzi—1994 | Aprili 1
-
-
6. Shetani alipingaje wema na enzi kuu ya Yehova?
6 Lakini Shetani alisema zaidi. Yeye aliendelea kusema hivi: “Kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” Kulingana na Shetani, Yehova Mungu—aliyekuwa amewaandalia wazazi wetu wa kwanza mengi sana—alitaka kuwanyima jambo fulani zuri ajabu. Alitaka kuwazuia wasiwe kama miungu. Hivyo, Shetani alipinga wema wa Mungu. Pia aliendeleza sifa ya kujiridhisha na kupuuza kimakusudi sheria za Mungu, akisema kwamba kutenda kwa njia hiyo kungekuwa na manufaa. Kwa kweli, Shetani alipinga enzi kuu ya Mungu juu ya uumbaji Wake mwenyewe, akidai kwamba Mungu hakuwa na haki ya kuwekea mipaka yale ambayo mwanadamu alifanya.
7. Mafundisho ya mashetani yalisikiwa lini kwa mara ya kwanza, nayo yanafananaje leo?
7 Kwa maneno hayo ya Shetani, mafundisho ya mashetani yalianza kusikiwa. Bado mafundisho hayo maovu huendeleza kanuni izo hizo zisizoonyesha kumwogopa Mungu. Kama vile alivyofanya katika bustani ya Edeni, bado Shetani pamoja na roho wengine walioasi ambao wamejiunga naye, hupinga haki ya Mungu ya kuweka viwango vya utendaji. Bado yeye hupinga enzi kuu ya Yehova na kujaribu kuwavuta wanadamu wasimtii Baba yao wa kimbingu.—1 Yohana 3:8, 10.
-
-
Ufundishaji wa Kimungu Dhidi ya Mafundisho ya MashetaniMnara wa Mlinzi—1994 | Aprili 1
-
-
13. Shetani ameambia wanadamu uwongo upi mbalimbali tangu Edeni?
13 Shetani alimshtaki Yehova kwa Hawa, kwamba alikuwa amesema uwongo naye Shetani akasema kwamba wanadamu wangeweza kuwa kama miungu ikiwa hawangemtii Muumba wao. Hali yenye dhambi ya wanadamu huthibitisha leo kwamba Shetani, wala si Yehova, ndiye aliyekuwa mwongo. Leo wanadamu si miungu! Hata hivyo, Shetani alifuatisha uwongo huo wa kwanza kwa uwongo mwingine. Alianzisha wazo la kwamba nafsi ya kibinadamu haiwezi kufa. Hivyo kwa njia ya kushawishi alitolea wanadamu uwezekano wa kuwa kama miungu kwa njia nyingine. Kisha, kwa msingi wa fundisho hilo bandia, aliendeleza mafundisho ya moto wa helo, purgatori, uwasiliani-roho, na ibada ya wazazi waliokufa. Bado uwongo huo mbalimbali umeshika mateka mamia ya watu.—Kumbukumbu la Torati 18:9-13.
-
-
Ufundishaji wa Kimungu Dhidi ya Mafundisho ya MashetaniMnara wa Mlinzi—1994 | Aprili 1
-
-
16. Ni nini matokeo ya muda mrefu wakati wanadamu wafuatapo hekima yao wenyewe?
16 Kwa uwongo wake katika bustani ya Edeni, Shetani aliwatia moyo Adamu na Hawa wajitahidi sana kutomtegemea Mungu na badala yake kutegemea hekima yao wenyewe. Leo, twaona matokeo ya muda mrefu ya hilo, katika uhalifu, magumu ya kiuchumi, vita, na ule ukosefu mkubwa sana wa usawa ulio katika ulimwengu leo. Si ajabu kwamba Biblia husema: “Hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu”! (1 Wakorintho 3:19) Hata hivyo, wanadamu wengi hupendelea kwa upumbavu kuteseka badala ya kutoa uangalifu kwa mafundisho ya Yehova. (Zaburi 14:1-3; 107:17) Wakristo, ambao wamekubali ufundishaji wa kimungu, huepuka kutumbukia katika mtego huo.
-