Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • “Uzao” Uliotabiriwa

      18. Ni unabii gani uliotolewa baada ya Adamu kutenda dhambi, na ni mambo gani yaliyofunuliwa baadaye kuhusu unabii huo?

      18 Katika Edeni, ilipoonekana kwamba wanadamu wamepoteza kila kitu, yaani, msimamo safi mbele za Mungu, uzima wa milele, furaha, na Paradiso—Yehova Mungu alitabiri kuja kwa Mkombozi. Mkombozi huyo alitajwa kuwa “uzao.” (Mwa. 3:15) Fumbo hilo kuhusu Uzao lilikuja kuwa msingi wa unabii mwingi wa Biblia kwa miaka mingi. Uzao huo ungetoka katika ukoo wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Pia, ungetoka katika ukoo wa Mfalme Daudi.—Mwa. 21:12; 22:16-18; 28:14; 2 Sam. 7:12-16.

      19, 20. (a) Ni nani aliye Uzao ulioahidiwa? (b) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba uzao uliotabiriwa unatia ndani watu wengine zaidi ya Yesu?

      19 Ni nani aliyekuwa Uzao huo ulioahidiwa? Jibu kwa swali hilo linaweza kupatikana kwenye Wagalatia 3:16. (Soma.) Hata hivyo, baadaye katika sura hiyohiyo, mtume Paulo anaendelea kuwaambia hivi Wakristo watiwa-mafuta: “Zaidi ya hayo, ikiwa ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu, warithi kuhusiana na ahadi.” (Gal. 3:29) Kwa kuwa wengine wanatiwa ndani, Kristo ni Uzao ulioahidiwa katika maana gani?

      20 Mamilioni ya watu wamedai kuwa wazao wa Abrahamu, wengine hata wamejifanya kuwa manabii. Dini fulani zinakazia kwamba manabii wake ni wazao wa Abrahamu. Lakini je, manabii wote hao ni Uzao ulioahidiwa? Hapana. Kama mtume Paulo anavyoonyesha kwa mwongozo wa roho ya Mungu, si wazao wote wa Abrahamu wanaoweza kudai kuwa Uzao ulioahidiwa. Wazao wa wana wengine wa Abrahamu hawakutumiwa kuwabariki wanadamu. Uzao wa baraka ungekuja kupitia tu Isaka. (Ebr. 11:18) Mwishowe, ni mwanadamu mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye ndiye sehemu ya msingi ya uzao uliotabiriwa, na Biblia inathibitisha kwamba alitokana na Abrahamu.c Wengine wote ambao baadaye walikuja kuwa sehemu ya pili ya uzao wa Abrahamu wanakubaliwa kwa sababu “ni wa Kristo.” Ndiyo, daraka la Yesu katika kutimiza unabii huo ni la pekee sana.

  • Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • c Hata ikiwa Wayahudi katika karne ya kwanza W.K. walifikiri kwamba walikuwa na kibali cha Mungu, kwa kuwa walikuwa watoto au wazao halisi wa Abrahamu, walitazamia kuja kwa mtu mmoja akiwa Masihi, au Kristo.—Yoh. 1:25; 7:41, 42; 8:39-41.

  • Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
    • ◼ Uzao Ulioahidiwa. (Mwa. 3:15) Ni mwanadamu mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye ndiye sehemu ya msingi ya uzao huo uliotabiriwa. Wengine wote ambao baadaye walikuja kuwa sehemu ya pili ya uzao wa Abrahamu “ni wa Kristo.”—Gal. 3:29.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki