-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Ulimwengu ulitoka wapi?
Biblia inasema: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Wanasayansi wengi wanakubali kwamba ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Mungu aliumbaje ulimwengu? Alitumia ‘nguvu yake ya utendaji,’ yaani, roho yake takatifu kuumba kila kitu ulimwenguni kutia ndani nyota na sayari.—Mwanzo 1:2.
-
-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Simulizi la Biblia kuhusu uumbaji linapatana na akili
Katika Mwanzo sura ya 1, Biblia inaeleza kuhusu chanzo cha dunia na uhai uliomo. Je, unaamini simulizi hilo, au je, ni hadithi ya kutungwa? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
Je, Biblia inafundisha kwamba dunia na uhai uliomo uliumbwa kwa siku sita zenye urefu wa saa 24?
Je, unafikiri simulizi la Biblia kuhusu uumbaji ni sahihi na linapatana na akili? Kwa nini?
Soma Mwanzo 1:1, kisha mzungumzie swali hili:
Wanasayansi wanasema kwamba ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Maoni yao yanapatanaje na jambo ambalo umesoma katika Biblia?
Baadhi ya watu hufikiri kwamba Mungu alitumia mageuzi kuumba uhai. Soma Mwanzo 1:21, 25, 27, kisha mzungumzie maswali haya:
Je, Biblia inafundisha kwamba Mungu aliumba uhai wa hali ya chini akauacha ujigeuze kuwa samaki, kisha mnyama, na mwishowe kuwa mwanadamu? Au je, aliumba “aina” mbalimbali za uhai?b
-