Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mambo Yaliyofunuliwa Ni Yetu Sisi”
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Mei 15
    • Siri za Yehova Zilizofunuliwa

      3. Ni ufunuo gani wa kusudi lake ambao Yehova alitolea Adamu na Hawa?

      3 Jambo la kufurahisha ni kwamba Yehova amekuwa akifunua maarifa kwa wingi sana. Tangu wakati wa uumbaji, Mungu amewapa waabudu wake hatua kwa hatua habari zote walizozihitaji chini ya hali mbalimbali. (Mithali 11:9; Mhubiri 7:12) Hapo kwanza, alieleza kwamba dunia na wanyama waliomo wangepaswa kuwa chini ya Adamu na Hawa na wazao wao. (Mwanzo 1:28, 29) Lakini, Shetani aliongoza Adamu na Hawa kwenye dhambi, na ikawa vigumu kuona ni jinsi gani kusudi la kimungu lingeweza kutimizwa limletee Mungu utukufu. Ingawa hivyo, Yehova alifanya haraka akaanza kueleza mambo. Alifunua kwamba, baada ya muda, kungetokea mzao mwadilifu, au “uzao,” ambao ungezipinga kazi za Shetani na wafuasi wake.—Mwanzo 3:15.

      4, 5. Ni mafunuo gani zaidi ambayo Yehova alitoa, na ni akina nani waliokuwa mifereji aliyoitumia?

      4 Bila shaka wanaume na wanawake wenye kumwogopa Mungu walikuwa na maulizo mengi juu ya Uzao huo. Yeye angekuwa nani? Angefika wakati gani? Angefaidije wanadamu? Karne zilipoendelea kupita, Yehova alitoa mafunuo zaidi juu ya makusudi yake, na hatimaye akajibu maulizo yote hayo. Kabla ya Gharika, alimwongoza Enoki kwa roho Yake atabiri katika unabii juu ya uharibifu uliokuwa unakuja wa uzao wa Shetani. (Yuda 14, 15) Karibu miaka 2,400 kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, alimkabidhi Noa ufunuo wa kwamba uhai na damu ya kibinadamu ni vitu vitakatifu—ukweli ambao ungekuwa wa maana kubwa wakati Uzao ulioahidiwa ungefika.—Mwanzo 9:1-7.

      5 Baada ya siku za Noa, Yehova alifunua maarifa yenye umaana mkubwa kwa kutumia wazee wengine waaminifu wa ukoo. Katika karne ya 20 K.W.K., Abrahamu alipata habari kwamba ule Uzao ulioahidiwa ungekuwa mmoja wa wazao wake. (Mwanzo 22:15-18) Ahadi hiyo ikawa mali yenye thamani kubwa sana ya Isaka mwanaye Abrahamu na Yakobo mjukuu wake (ambaye baadaye aliitwa Israeli). (Mwanzo 26:3-5; 28:13-15) Halafu, kupitia Yakobo, Yehova akafunua kwamba huyo aliye Uzao, “Shilo,” angekuwa mtawala mwenye uwezo mwingi ambaye angezaliwa katika ukoo wa Yuda mwanaye.—Mwanzo 49:8-10.

  • “Mambo Yaliyofunuliwa Ni Yetu Sisi”
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Mei 15
    • 7, 8. (a) Ni habari gani zaidi ambazo Yehova alifunua juu ya Uzao uliokuwa unakuja? (b) “Mambo yaliyofunuliwa” yalihifadhiwaje, na ni nani aliyefunua ufahamu unaofaa juu ya mambo hayo?

      7 Wakati uliozidi kupita, Yehova alitoa mafunuo zaidi juu ya ule Uzao. Kupitia mtunga zaburi, Mungu alifunua kwamba mataifa yangeukataa Uzao wake lakini kwamba Uzao huo ungeshinda kwa msaada wa Yehova. (Zaburi 2:1-12) Kupitia Isaya, alifunua kwamba Uzao huo ungekuwa ndiye yule “Mwana-Mfalme” lakini kwamba angetaabika pia kwa ajili ya dhambi za wengine. (Isaya 9:6, NW; 53:3-12, UV ) Katika karne ya nane K.W.K., Yehova hata alifunua ni wapi Uzao huo ungezaliwa na, katika karne ya sita K.W.K., akafunua ratiba ya wakati ya huduma yake.—Mika 5:2; Danieli 9:24-27.

  • “Mambo Yaliyofunuliwa Ni Yetu Sisi”
    Mnara wa Mlinzi—1986 | Mei 15
    • 11, 12. Ni nini yaliyokuwa baadhi ya mafunuo mazuri ajabu yaliyotolewa kupitia mfereji huo mpya?

      11 Uhakika mkubwa wa hizo ‘siri takatifu’ mpya ulikuwa kwamba Yesu Kristo, ule Uzao ulioahidiwa, alikuwa ametokea. (Wagalatia 3:16) Yesu alikuwa ndiye “Shilo,” yule mwenye haki ya kutawala wanadamu, na Yehova alimweka rasmi awe Mfalme wa Ufalme ambao hatimaye ungerudisha Paradiso kwenye dunia hii. (Isaya 11:1-9; Luka 1:31-33) Yesu alikuwa pia ndiye Kuhani Mkuu aliyewekwa rasmi na Yehova, ambaye alitoa uhai wake mkamilifu usio na kidoa uwe ukombozi kwa ajili ya wanadamu, hayo yakiwa ni matumizi mazuri ajabu ya ile kanuni ya utakatifu wa damu. (Waebrania 7:26; 9:26) Tangu wakati huo, wanadamu wenye kuamini walikuwa na tumaini la kupata tena uhai mkamilifu wa kibinadamu uliopotezwa na Adamu.—1 Yohana 2:1, 2.

      12 Huyo aliye Uzao ulioahidiwa alikuwa mpatanishi pia, mwenye kutendesha kazi kati ya wafuasi wake na Babaye wa kimbingu agano jipya lililochukua mahali pa lile agano la kale la Torati. (Waebrania 8:10-13; 9:15) Kwa kutegemea msingi wa agano jipya hili, kundi changa la Kikristo lilichukua mahali pa taifa la Israeli wa kimwili, likawa Israeli wa kiroho, ‘uzao wa Abrahamu’ wa kiroho pamoja na Yesu, na mawakili wa “mambo yaliyofunuliwa.” (Wagalatia 3:29; 6:16; 1 Petro 2:9) Zaidi ya hilo, watu wa mataifa walialikwa wawe sehemu ya Israeli huyo wa kiroho—jambo lisilowazika kwa Wayahudi! (Warumi 2:28, 29) Wakiwa pamoja, Waisraeli wa kiroho walio Wayahudi na wasio Wayahudi waliagizwa wafanye wanafunzi wa Yesu katika sehemu zote za dunia. (Mathayo 28:19, 20) Hivyo, “mambo yaliyofunuliwa” yakawa yanahusu mataifa yote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki