-
“Acheni Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Aprili
-
-
12. Tunajifunza nini kutokana na mfano wa makerubi waliowekwa katika Edeni?
12 Makerubi. Mfano uliowekwa na baadhi ya viumbe wa roho wa kwanza kuonekana kwa wanadamu, unaweza kutufundisha kuwa wavumilivu tunapopata mgawo mgumu. Yehova Mungu “akaweka upande wa mashariki wa bustani ya Edeni makerubi na upanga unaowaka ambao ulikuwa unajizungusha-zungusha ili kuilinda njia ya kwenda kwenye ule mti wa uzima.”[2] (Mwa. 3:24) Ni wazi kwamba makerubi hao hawakuumbwa kwa kusudi la kupewa mgawo huo! Kwa kweli, dhambi na uasi haukuwa sehemu ya kusudi la Yehova kwa wanadamu. Hata hivyo, hatusomi popote kwamba makerubi, viumbe wa roho wenye cheo cha juu, walilalamika kwamba kazi waliyopewa ilikuwa ya hali ya chini sana. Hawakuchoka wala kukata tamaa. Badala yake, walishikamana kwa utiifu na mgawo wao na kuvumilia kwa zaidi ya miaka 1,600 hadi kazi yao ilipokwisha, labda wakati wa Gharika!
-
-
“Acheni Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Aprili
-
-
^ [2] (fungu la 12) Biblia haisemi ni makerubi wangapi walipewa kazi hiyo.
-