-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 1
-
-
Ikiwa ndivyo, alikuwa amekosea sana. Zaidi ya hayo, ikiwa yeye na Adamu walimwambia Kaini mambo kama hayo alipokuwa mvulana, kwa kweli walimfanya awe na kiburi. Baada ya muda, Hawa alizaa mwana wa pili, lakini hatusomi maneno ya kumsifu. Walimwita Abeli, jina linalomaanisha “Pumzi,” au “Ubatili.” (Mwanzo 4:2) Je, jina hilo linamaanisha kwamba hawakutazamia mengi kutoka kwake, kana kwamba walikuwa na matumaini mengi zaidi katika Kaini kuliko Abeli? Labda walifikiri hivyo.
-
-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 1
-
-
Wavulana hao walipoendelea kukua, inaelekea Adamu aliwazoeza kufanya kazi ambayo ingesaidia familia kupata mahitaji. Kaini alifanya kazi ya ukulima, naye Abeli akafanya kazi ya kuchunga wanyama.
-
-
“Ijapokuwa Alikufa, Bado Anasema”Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 1
-
-
Bila shaka, Abeli alitenga wakati wa kufikiria mambo ya kiroho. Mwazie akichunga wanyama wake. Mchungaji alihitaji kutembea sana. Aliwaongoza wanyama kwenye vilima, mabonde, kuvuka mito, kila mara akitafuta majani mabichi zaidi, chemchemi bora za kunywesha wanyama, na mahali salama zaidi pa kupumzikia. Kati ya viumbe wote wa Mungu, inaonekana kondoo ndio waliohitaji kuchungwa, kana kwamba waliumbwa wakiwa na uhitaji wa kuongozwa na kulindwa na mwanadamu. Je, Abeli aliona kwamba yeye pia alihitaji mwongozo, ulinzi, na utunzaji kutoka kwa Mtu mwenye hekima na uwezo zaidi kuliko wanadamu? Bila shaka, alitaja mambo kama hayo katika sala, na hivyo imani yake ikaendelea kukua.
Kwa kutazama uumbaji, Abeli alipata msingi wa kuwa na imani thabiti katika Muumba
-