Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mungu Alikubali” Zawadi Zao
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Abeli Alituwekea Mfano Kuhusu Ibada Safi

      10. Abeli alituwekeaje mfano mzuri kuhusu ibada safi?

      10 Abeli alimtolea Yehova dhabihu yake, akijua kwamba Yehova peke yake ndiye anayestahili kuipokea. Alitoa dhabihu bora​—Abeli alichagua “baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake.” Ingawa Biblia haisemi kama alitoa dhabihu yake kwenye madhabahu, ni wazi kwamba njia aliyotumia ilikubalika. Lakini jambo muhimu kuhusu zawadi ya Abeli ni nia yake ya kutoa, mfano ambao karibu miaka 6,000 baadaye bado tunapaswa kuuiga. Abeli alichochewa na imani yake katika Mungu na upendo wake kwa viwango vya uadilifu vya Yehova. Tunajuaje?

      Abeli akiwa mbele ya madhabahu, akitoa dhabihu kwa Yehova. Nyuma yake, makerubi wakiwa wamefunga njia ya kuingia kwenye bustani ya Edeni.

      Abeli alitimiza mambo manne muhimu yanayohitajiwa katika ibada safi (Tazama fungu la 10)

      11. Kwa nini Yesu alisema kwamba Abeli alikuwa mwadilifu?

      11 Kwanza, fikiria jambo ambalo Yesu alisema kumhusu Abeli. Yesu alimfahamu vizuri. Yesu alikuwa mbinguni Abeli alipokuwa hai. Yesu alimpenda sana mwana huyo wa Adamu. (Met. 8:22, 30, 31; Yoh. 8:58; Kol. 1:15, 16) Basi, Yesu alikuwa akitoa ushahidi aliojionea aliposema kwamba Abeli alikuwa mwadilifu. (Mt. 23:35) Mtu mwadilifu anakubali kwamba Yehova ndiye anayepaswa kuweka viwango vya mema na mabaya. Lakini anafanya mengi zaidi—anaonyesha kwa maneno na matendo kwamba anakubaliana na viwango hivyo. (Linganisha Luka 1:5, 6.) Muda unahitajiwa ili mtu ajulikane kuwa mwadilifu. Hata kabla hajamtolea Mungu zawadi, Abeli alijulikana kuwa mtu aliyeishi kulingana na viwango vya Yehova. Haikuwa rahisi kwake kuwa mwadilifu. Inawezekana kwamba ndugu yake mkubwa hakumsaidia kwa kuwa moyo wa Kaini ulikuwa mwovu. (1 Yoh. 3:12) Mama yake Abeli alikosa kutii amri ya Mungu, na baba yake alikuwa amemwasi Yehova, akitaka kujiamulia mema na mabaya. (Mwa. 2:16, 17; 3:6) Abeli alionyesha ujasiri mkubwa kwa kuishi kwa njia tofauti na familia yake!

      12. Kulikuwa na tofauti gani kubwa kati ya Kaini na Abeli?

      12 Kisha, fikiria jinsi mtume Paulo anavyohusianisha sifa ya imani na uadilifu. Aliandika hivi: “Kwa imani, Abeli alimtolea Mungu dhabihu ya thamani kubwa zaidi kuliko ile ya Kaini, na kupitia imani hiyo alitolewa ushahidi kwamba alikuwa mwadilifu.” (Ebr. 11:4) Maneno ya Paulo yanaonyesha kwamba tofauti na Kaini, Abeli alichochewa na imani thabiti katika Yehova na njia yake ya kufanya mambo.

      13. Mfano wa Abeli unatufundisha nini?

      13 Mfano wa Abeli unatufundisha kwamba ibada safi inatoka tu katika moyo wenye nia nzuri​—moyo uliojaa imani katika Yehova na unaokubaliana kabisa na viwango vyake vya uadilifu. Isitoshe, tunajifunza kwamba ibada safi haihusishi tendo moja tu la ibada. Inahusisha maisha yetu yote, mwenendo wetu wote.

  • “Mungu Alikubali” Zawadi Zao
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki