-
Kumtolea Yehova Dhabihu Zenye KukubalikaMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 1
-
-
Baada ya muda fulani, yaelekea walipofikia umri wa utu mzima kabisa, Kaini na Abeli walitoa kila mmoja wao dhabihu kwa Yehova. Kwa kuwa Abeli alikuwa mchungaji, haishangazi kwamba yeye alitoa “wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama.” Tofauti na Abeli, Kaini alitoa “mazao ya ardhi.” Yehova aliikubali dhabihu ya Abeli, bali “Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake.” (Mwanzo 4:3-5) Kwa nini?
Wengine huonyesha uhakika wa kwamba dhabihu ya Abeli ilitokana na “wazao wa kwanza wa wanyama wake,” ilhali ya Kaini ilikuwa tu “mazao ya ardhi.” Lakini tatizo halikuwa ubora wa mazao ambayo Kaini alitoa, kwa kuwa simulizi hilo lasema kwamba Yehova alimtakabali ‘Abeli na sadaka yake,’ bali “Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake.” Kwa hiyo, Yehova alitazama hasa hali ya moyo ya mwabudu huyo. Ni nini alichotambua kwa kufanya hivyo? Andiko la Waebrania 11:4 lasema kwamba Abeli alitoa dhabihu yake “kwa imani.” Kwa hiyo, yaonekana dhabihu ya Kaini ilikosa imani iliyofanya dhabihu ya Abeli ikubaliwe.
Kwa habari hiyo, yafaa kuangaliwa kwamba dhabihu ya Abeli ilihusisha kumwagwa damu. Huenda akawa kwa kufaa alikata kauli kwamba ahadi ya Mungu kuhusu mbegu ambaye angepondwa kisigino ingehusisha dhabihu ya uhai. Hivyo, dhabihu ya Abeli ingekuwa ombi la kufunika, nayo ilionyesha imani kwamba Mungu angetoa dhabihu yenye kufunika dhambi katika wakati ufaao.
-
-
Kumtolea Yehova Dhabihu Zenye KukubalikaMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 1
-
-
Biblia haionyeshi jinsi ambavyo Yehova alionyesha kibali chake kwa dhabihu ya Abeli. Wengine hudokeza kwamba ilichomwa kabisa kwa moto kutoka mbinguni. Kwa vyovyote vile, alipong’amua kwamba dhabihu yake imekataliwa, “Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.” (Mwanzo 4:5) Kaini alikuwa akielekea kupatwa na msiba.
-