-
Kitabu Cha Biblia Namba 1—Mwanzo“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
33. Taja kanuni na mazoea fulani ya jumuiya ya wazee wa ukoo yaliyo ya maana katika kuielewa Biblia.
33 Pia lenye mafaa halisi kwa mwanafunzi wa Maandiko ni kuchunguza jumuiya ya wazee wa ukoo ambayo Mwanzo hueleza. Jumuiya ya wazee wa ukoo ilikuwa namna ya ujamii wa serikali ya familia iliyokuwako miongoni mwa watu wa Mungu tangu siku ya Nuhu hadi kutolewa kwa Sheria kwenye Mlima Sinai. Mengi ya maelezo yaliyotiwa ndani ya agano la Sheria yalikuwa tayari yakizoewa katika jumuiya ya wazee wa ukoo. Kanuni kama ustahili wa kijumuiya (18:32), daraka la kijumuiya (19:15), adhabu ya kifo na pia utakatifu wa damu na wa uhai (9:4-6), na chuki ya Mungu juu ya kutukuzwa kwa wanadamu (11:4-8) yamekuwa na matokeo juu ya ainabinadamu katika historia yote. Mazoea na semi nyingi za kisheria zinaangaza juu ya matukio ya baadaye, hata kufikia siku za Yesu. Sheria ya wazee wa ukoo inayaosimamia kutunza watu na mali (Mwa. 31:38, 39; 37:29-33; Yn. 10:11, 15; 17:12; 18:9) na jinsi ya kupokeza mali (Mwa. 23:3-18), na pia sheria inayoongoza urithi wa mtu aliyepokea haki ya mzaliwa wa kwanza (48:22), lazima ijulikane ikiwa tutakuwa na msingi unaohitajiwa ili kuelewa wazi Biblia. Mazoea mengine ya jumuiya ya wazee wa ukoo yaliyotiwa katika Sheria yalikuwa dhabihu, tohara (aliyopewa Abrahamu kwanza), ufanyaji wa maagano, ndoa ya ndugu-mkwe (38:8, 11, 26), na utumizi wa viapo ili kuthibitisha jambo.—22:16; 24:3.f
-