-
Ukweli Kuhusu Simulizi la UumbajiAmkeni!—2014 | Machi
-
-
MUNGU ALITUMIA MUDA GANI KUUMBA ULIMWENGU?
Biblia inasema kwamba Mungu aliumba “mbingu na dunia.” Maneno hayo yenye maana pana hayataji kipindi kilichohusika kuumba ulimwengu wote au njia iliyotumiwa kuutokeza. Namna gani madai ya wanauumbaji wanaosema kwamba Mungu aliumba ulimwengu kwa siku sita zenye urefu wa saa 24 kila moja? Wazo hilo linalopingwa vikali na wanasayansi linategemea ufafanuzi usio sahihi kuhusu simulizi hilo la Biblia. Acheni tuchunguze yale ambayo Biblia inasema.
Biblia haiungi mkono watu wenye imani kali wala wanauumbaji wanaodai kwamba dunia iliumbwa kwa siku sita zenye urefu wa saa 24 kila moja
-