-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Ni nini kinachofanya wanadamu wawe tofauti na wanyama?
Baada ya kuumba dunia, Yehova aliumba viumbe. Kwanza, aliumba mimea na wanyama duniani. Kisha, “Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake.” (Soma Mwanzo 1:27.) Kwa nini wanadamu ni viumbe wa kipekee? Tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, kwa hiyo tunaweza kuonyesha sifa zake kama vile upendo na haki. Vilevile alituumba tukiwa na uwezo wa kujifunza lugha, kufurahia vitu maridadi, na muziki. Tofauti na wanyama, tunaweza kumwabudu Muumba wetu.
-
-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Wanadamu ni viumbe wa kipekee wa Mungu
Sisi ni tofauti na wanyama ambao Yehova aliumba. Soma Mwanzo 1:26, kisha mzungumzie swali hili:
Kwa kuwa tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, uwezo wetu wa kuonyesha upendo na huruma unatufundisha Mungu ana sifa gani?
-