Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwe na Imani Kama ya Abrahamu!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 15
    • 10. Ni tatizo gani lililotokea baina ya wachungaji wa Abramu na Loti, na ni kwa nini ilifaa tatizo hilo lisuluhishwe haraka?

      10 ‘Na Loti aliyesafiri pamoja na Abramu, yeye naye alikuwa na makundi ya ng’ombe na kondoo, na hema. Na ile nchi haikuwatosha, ili wakae pamoja; maana mali zao zilikuwa nyingi, hata wasiweze kukaa pamoja. Kukawako ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abramu na, wachunga wanyama wa Loti; na siku zile Wakaanani na Waperizi walikuwa wakikaa katika nchi.’ (Mwanzo 13:5-7) Nchi hiyo haikuwa na maji wala malisho ya kutosha mifugo ya Abramu na ya Loti. Hivyo kukawa na ugomvi na chuki baina ya wachungaji hao. Haikufaa waabudu wa Mungu wa kweli kugombana. Iwapo ugomvi huo ungeendelea, uhusiano wao ungevunjika kabisa. Hivyo Abramu angesuluhishaje ugomvi huo? Alikuwa amechukua Loti baada ya kifo cha baba ya Loti, na labda kumlea kama mtoto wake mwenyewe. Kwa kuwa Abramu ndiye aliyekuwa na umri mkubwa zaidi kati yao wawili, je hakustahili kuchukua kilichokuwa bora zaidi?

      11, 12. Abramu alimtolea Loti pendekezo gani la ukarimu, na ni kwa nini uchaguzi wa Loti haukuwa wa hekima?

      11 Lakini ‘Abramu akamwambia Loti, Basi, usiwepo ugomvi, nakusihi, kati ya mimi na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako; maana sisi tu ndugu. Je! Nchi hii yote haiko mbele yako? Basi ujitenge nami, nakusihi; ukienda upande wa kushoto, nitakwenda upande wa kuume; ukienda upande wa kuume, nitakwenda upande wa kushoto.’ Karibu na Betheli kuna ile ambayo imetajwa kuwa “sehemu nzuri sana ya kutazama eneo la Palestina.” Labda ni kutoka hapo ‘Loti aliinua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla BWANA hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa kama bustani ya BWANA, kama nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.’—Mwanzo 13:8-10.

  • Mwe na Imani Kama ya Abrahamu!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 15
    • 13. Kielelezo cha Abramu chaweza kuwasaidiaje Wakristo ambao huenda wakawa na ugomvi wa kifedha?

      13 Lakini Abramu alionyesha imani katika ahadi ya Yehova kwamba hatimaye mbegu yake ingemiliki nchi hiyo yote; hakugombania sehemu ndogo tu ya nchi hiyo. Kwa ukarimu, yeye alitenda kupatana na kanuni ambayo baadaye ilitajwa kwenye 1 Wakorintho 10:24: “Acheni kila mmoja afulize kutafuta sana, si faida yake mwenyewe, bali ya mtu yule mwingine.” Hili ni kikumbusho kizuri kwa wale ambao huenda wakawa na ugomvi wa kifedha na waamini wenzao. Badala ya kufuata ushauri ulio kwenye Mathayo 18:15-17, wengine wamepeleka ndugu zao mahakamani. (1 Wakorintho 6:1, 7) Kielelezo cha Abramu chaonyesha kwamba ni afadhali kupata hasara kifedha badala ya kufanya jina la Yehova lishutumiwe au kuharibu amani ya kutaniko la Kikristo.—Yakobo 3:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki