-
Abrahamu—Mnabii na Rafiki ya MunguMnara wa Mlinzi—1989 | Julai 1
-
-
MAJESHI yaliyoungana ya wafalme wanne wa Mashariki yanavuka Mto Eufrati. Njia wanayofuata wakipiga miguu ni Njia Kuu ya Mfalme kuelekea upande wa mashariki wa bonde la Mto Yordani. Wakiwa mwendoni wanawashinda Warefaimu, Wazuzimu, Waemimu, na Wahori. Halafu, wavamizi hao wanageuka na kushinda wakaaji wote wa Negebu ya kusini.
Ni nini kusudi la kampeni hii ya kijeshi? Kitu wanachokitaka sana kimo katikati ya majimbo yale yaliyovamiwa ng’ambo ya Yordani na ile Negebu. Kitu chenyewe ni bonde fulani lenye kutamaniwa sana linaloitwa Wilaya ya Yordani. (Mwanzo 13:10) Hapa, wakaaji wa mikoa mitano ambayo ni majiji, Sodoma, Gomora, Adma, Seboimu, na Bela, wanaishi maisha ya kizembe tu yenye starehe za vitu vya kimwili. (Ezekieli 16:49, 50) Wakati mmoja walikuwa wametiishwa chini ya aliyeonekana kuwa kiongozi wa majeshi hayo yaliyounganika, Kedorlaoma, mfalme wa Elamu. Lakini wameasi dhidi yake. Sasa, wanakabiliwa na utozwaji hesabu, bila msaada wa majirani. Kedorlaoma na waungani wake wanashinda pigano linalotokea na kuanza mwendo wao mrefu wa kupiga miguu kwenda nyumbani wakiwa na nyara nyingi.
Miongoni mwa watekwa yumo mwanamume mwadilifu, Loti. Yeye ni mpwa-mume wa Abrahamu, ambaye amepiga hema katika milima ya karibu ya Hebroni. Abrahamu anaposikia habari hizo za kutaabisha sana, mara hiyo anaita watu 318 kati ya wanaume wake. Wakiwa na usaidizi wa majirani fulani, kwa ushujaa wanawafuata mbio wafalme hao wanne na kufumania majeshi yao usiku. Wavamizi hao wanakimbia. Loti na watu wa nyumba yake wanaponyolewa, pamoja na watekwa wengine na bidhaa.
Sisi tuna sababu gani ya kuamini kumbukumbu hili la maandishi yaliyo katika sura ya 14 ya Mwanzo? Je! hadithi hii ilivumbuliwa tu ili kumfanya baba mtangulizi wa mataifa kadhaa, kutia na Wayahudi, awe shujaa wa kitaifa? Namna gani matukio mengine katika maisha ya Abrahamu?
-
-
Abrahamu—Mnabii na Rafiki ya MunguMnara wa Mlinzi—1989 | Julai 1
-
-
Uvamizi wa Kedorlaoma
Namna gani ushindi wa Abrahamu juu ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu? Mapema katika karne ya 19, ni machache yaliyojulikana juu ya Waelami. Wachambuzi wa Biblia walilikataa wazo la kwamba Elamu alipata kuwa na uvutano juu ya Babuloni, achia mbali Palestina. Sasa, Waelami wanaonwa kwa njia tofauti. Uchimbuzi wa vitu vya kale unawafunua kwamba walikuwa taifa la kivita lenye nguvu. Funk & Wagnalls Standard Reference Encyclopedia inataarifu hivi: “Waelami waliharibu jiji la Uru karibu 1950 K.K. . . . Baada ya hapo walitokeza uvutano wa kadiri kubwa juu ya watawala wa Babulonia.”
Tena, majina ya wafalme Waelami yamepatikana juu ya miandiko iliyochorwa juu ya machimbuo ya kale. Baadhi ya majina hayo yanaanza kwa neno “Kuduri,” linalofanana na “Kedori.” Mungumke Mwelami aliye wa maana alikuwa Lagamari, neno linalofanana na “laoma.” Hivyo, Kedorlaoma anakubaliwa sasa na vyanzo fulani vya kilimwengu kwamba alikuwa mtawala wa kihistoria, kukiwa na uwezekano wa kwamba jina lake lilimaanisha “Mtumishi wa Lagamari.” Fungu moja la miandiko ya Kibabulonia lina majina yanayofanana na watatu kati ya wale wafalme wenye kuvamia—Tudhula (Tidali), Eriaku (Arioki), na Kuduru-lahmili (Kedorlaoma). (Mwanzo 14:1) Katika kitabu Hidden Things of God’s Revelation, Dakt. A. Custance anaongezea hivi: “Zaidi ya majina haya yalikuwako maelezo madogo-madogo yaliyoelekea kutaja matukio yaliyotendeka katika Babulonia wakati Waelami waliposimamisha imara enzi kuu yao juu ya nchi hiyo. . . . Tableti hizi zililithibitisha sana Andiko hata Wachambuzi wa Juu Zaidi wakazirukia na kufanya kila waliloweza ili waugandamize kwa makusudi umaana wazo.”
-