-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Ni nini kinachofanya wanadamu wawe tofauti na wanyama?
Baada ya kuumba dunia, Yehova aliumba viumbe. Kwanza, aliumba mimea na wanyama duniani. Kisha, “Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake.” (Soma Mwanzo 1:27.) Kwa nini wanadamu ni viumbe wa kipekee? Tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, kwa hiyo tunaweza kuonyesha sifa zake kama vile upendo na haki. Vilevile alituumba tukiwa na uwezo wa kujifunza lugha, kufurahia vitu maridadi, na muziki. Tofauti na wanyama, tunaweza kumwabudu Muumba wetu.
-
-
Uhai Ulianzaje?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Simulizi la Biblia kuhusu uumbaji linapatana na akili
Katika Mwanzo sura ya 1, Biblia inaeleza kuhusu chanzo cha dunia na uhai uliomo. Je, unaamini simulizi hilo, au je, ni hadithi ya kutungwa? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
Je, Biblia inafundisha kwamba dunia na uhai uliomo uliumbwa kwa siku sita zenye urefu wa saa 24?
Je, unafikiri simulizi la Biblia kuhusu uumbaji ni sahihi na linapatana na akili? Kwa nini?
Soma Mwanzo 1:1, kisha mzungumzie swali hili:
Wanasayansi wanasema kwamba ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Maoni yao yanapatanaje na jambo ambalo umesoma katika Biblia?
Baadhi ya watu hufikiri kwamba Mungu alitumia mageuzi kuumba uhai. Soma Mwanzo 1:21, 25, 27, kisha mzungumzie maswali haya:
Je, Biblia inafundisha kwamba Mungu aliumba uhai wa hali ya chini akauacha ujigeuze kuwa samaki, kisha mnyama, na mwishowe kuwa mwanadamu? Au je, aliumba “aina” mbalimbali za uhai?b
-