-
Yesu KristoUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Bila shaka katika pindi nyingi wakati wa maisha yake kabla ya kuwa binadamu akiwa yule Neno, Yesu alitenda akiwa Msemaji wa Yehova kwa watu walioko duniani. Ingawa maandiko fulani humrejezea Yehova ni kana kwamba anaongea moja kwa moja na binadamu, maandiko mengine huonyesha wazi kwamba alifanya hivyo kupitia mwakilishi wa kimalaika. (Linganisha Kut 3:2-4 na Mdo 7:30, 35; pia Mwa 16:7-11, 13; 22:1, 11, 12, 15-18.) Kusababu kuzuri ni kwamba katika visa vilivyo vingi kati ya hivyo, Mungu aliongea kupitia huyo Neno. Inaelekea yeye alifanya hivyo katika Edeni, kwa maana katika mbili kati ya zile pindi tatu zinazotaja Mungu akiongea hapo, maandishi yanaonyesha kihususa kuna mtu fulani aliyekuwa pamoja Naye, bila shaka Mwanaye. (Mwa 1:26-30; 2:16, 17; 3:8-19, 22) Basi, inawezekana kwamba Mwana wa Mungu, yule Neno, ndiye aliyekuwa malaika aliyeongoza Israeli kupita nyikani na ambaye sauti yake Waisraeli walipaswa kuitii kikiki kwa sababu ‘jina la Yehova lilikuwa ndani yake.’—Kut 23:20-23; linganisha Yos 5:13-15.
-
-
Mikaeli Yule Malaika Mkuu Ni Nani?Mnara wa Mlinzi—2005 | Machi 1
-
-
Mikaeli Yule Malaika Mkuu Ni Nani?
GABRIELI na Mikaeli ndio malaika pekee watakatifu wanaotajwa kwa jina katika Biblia, na Mikaeli tu ndiye anayeitwa “malaika mkuu.” (Yuda 9) Jina hilo linatajwa mara ya kwanza katika sura ya kumi ya Danieli, ambako Mikaeli anatajwa kuwa “mmoja wa hao wakuu wa mbele”; alikuja kumsaidia malaika mdogo ambaye alipingwa na “mkuu wa ufalme wa Uajemi.” Mikaeli aliitwa ‘mkuu wa watu wa Danieli,’ “yule mkuu anayesimama kwa ajili ya wana wa watu [wa Danieli].” (Danieli 10:13, 20, 21; 12:1) Hilo linaonyesha kwamba Mikaeli ndiye malaika aliyewaongoza wana wa Israeli nyikani. (Kutoka 23:20, 21, 23; 32:34; 33:2) Jambo linalounga mkono kauli hiyo ni kwamba ‘Mikaeli, yule malaika mkuu alikuwa na tofauti na Ibilisi na kubishana naye juu ya mwili wa Musa.’—Yuda 9.
-