Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ni Nani Ameijua Akili ya Yehova?”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • 14. Musa alitenda jinsi gani baada ya kusikia maneno ya Yehova?

      14 Simulizi hilo linaendelea kusema hivi: “Musa akaanza kuutuliza uso wa Yehova Mungu wake na kusema: ‘Kwa nini, Ee Yehova, hasira yako iwake juu ya watu wako ambao uliwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu? Kwa nini Wamisri waseme, “Aliwatoa kwa nia mbaya ili awaue katikati ya milima na kuwaangamiza kutoka katika uso wa nchi”? Geukia mbali uiache hasira yako inayowaka na ujute kuhusu uovu huo juu ya watu wako. Wakumbuke Abrahamu, Isaka na Israeli watumishi wako, uliowaapia kwa jina lako mwenyewe, kwa kuwa uliwaambia, “nitauzidisha uzao wenu kama nyota za mbinguni, nayo nchi hii yote ambayo nimeichagua, nitaupa uzao wenu, ili kwa kweli wapate kuimiliki mpaka wakati usio na kipimo.”’ Naye Yehova akaanza kujuta juu ya ule uovu aliokuwa amesema kwamba atawafanyia watu wake.”—Kut. 32:11-14.a

  • “Ni Nani Ameijua Akili ya Yehova?”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • 16 Jibu la Musa lilionyesha kwamba alikuwa na imani na uhakika katika haki ya Yehova. Jibu lake lilionyesha kwamba hakuwa na ubinafsi, lakini alihangaikia jina la Yehova. Hakutaka jina hilo liharibiwe sifa. Hivyo basi, Musa alionyesha kwamba alielewa “akili ya Yehova” kuhusu jambo hilo. (1 Kor. 2:16) Matokeo yalikuwa nini? Kwa sababu Yehova hakuwa ameamua kabisa kuchukua hatua fulani, simulizi hilo lililoongozwa na roho ya Mungu linasema kwamba ‘alianza kujuta.’ Katika Kiebrania, maneno hayo yanaweza kumaanisha tu kwamba Yehova hakuleta msiba ambao inaelekea angeleta juu ya taifa lote.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki