-
Je! Ye Yote Ameona Mungu?Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
-
-
Wakati Musa aliponena na Mungu “uso kwa uso,” kama inavyotaarifiwa kwenye Kutoka 33:11, NW, yeye hakuwa katika mawasiliano ya kuonana na Yehova. Usemi huo unaonyesha namna ambayo katika hiyo Musa aliwasiliana na Mungu, si kile ambacho yeye aliona. Kunena na Mungu “uso kwa uso” kunaonyesha maongezi kati ya watu wawili. Vivyo hivyo, mtu anaweza kuendesha maongezi kati yake na mwingine kwa simu, bila kuona mtu yule mwingine.
Musa alipoongea na Mungu na kupokea maagizo kutoka kwake, mawasiliano hayo hayakuwa kupitia njozi, kama ilivyokuwa mara nyingi kwa habari ya manabii wengine. Jambo hilo linaonwa kwenye Hesabu 12:6-8, ambapo sisi tunasoma: “Yeye aliendelea kusema: ‘Sikieni maneno yangu, tafadhali. Kama kungekuja kuwa na nabii wenu kwa ajili ya Yehova, ingekuwa ni katika njozi mimi ningejijulisha mwenyewe kwake. Katika ndoto mimi ningenena naye. Si hivyo Musa mtumishi wangu! Yeye anaitibarishwa nyumba yangu yote. Kinywa kwa kinywa mimi ninanena naye, hivyo nikimwonyesha yeye, wala si kwa vitendawili; na sura ya Yehova ndicho kitu ambacho yeye anaangalia.’” Ni katika maana gani Musa aliangalia “sura ya Yehova”?
-
-
Je! Ye Yote Ameona Mungu?Mnara wa Mlinzi—1988 | Mei 15
-
-
Kwamba Musa kwa kweli alinena na malaika aliyekuwa anawakilisha Mungu kibinafsi inaonyeshwa pia kwenye Matendo 7:38 (NW), inayotaarifu hivi: “Huyu ndiye yule ambaye alikuja kuwa miongoni mwa lile kundi katika jangwa pamoja na malaika ambaye alinena naye juu ya Mlima Sinai na pamoja na baba zetu wa kwanza-kwanza.” Malaika huyo alikuwa mnenaji wa kibinafsi kwa ajili ya Yehova Mungu, Muumba, na kwa hiyo yeye alinena na Musa kama kwamba ni Mungu mwenyewe aliyekuwa akinena.
-